Hamia kwenye habari

Igeni Imani Yao​—Wanaume na Wanawake Katika Biblia

Mfululizo huu unazungumzia maisha ya wanaume na wanawake wanaotajwa katika Biblia waliokuwa na imani ya pekee. a Masimulizi yao yaliyo katika Biblia ya jinsi walivyoonyesha imani, yanaweza kuimarisha imani yako na kukusaidia kumkaribia Mungu.

a Ili kukusaidia kupiga picha na kuzama kabisa katika masimulizi hayo ya watu walioonyesha imani, makala zilizo katika mfululizo huu zinatia ndani habari ambazo hazipatikani katika Biblia. Habari hizo hufanyiwa utafiti kwa makini sana ili kuhakikisha kwamba zinapatana na simulizi la Biblia na habari za kihistoria na uchunguzi wa vitu vya kale

Kuanzia Uumbaji Hadi Gharika

Abeli​—“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”

Tunaweza kujifunza nini kumhusu Abeli na imani yake ingawa Biblia haisemi mengi kumhusu?

Enoko​—‘Alimpendeza Mungu Vema’

Ikiwa wewe ni kichwa cha familia au unakabili changamoto ya kudumisha msimamo wako wa kile unachoamini kuwa sahihi, unaweza kujifunza mengi kutokana na imani ya Enoko.

Noa—“Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”

Noa na mke wake walikabili matatizo gani katika kuwalea watoto wao? Walionyeshaje imani kwa kujenga safina?

Noa Alilindwa Akiwa “Salama Pamoja na Wengine Saba”

Noa na familia yake waliokokaje kipindi kigumu zaidi katika historia ya wanadamu?

Kuanzia Gharika Hadi Kutoka

Abramu​—“Baba ya Wale Wote Walio na Imani”

Abramu alionyeshaje imani? Ungependa kuiga imani ya Abramu katika njia zipi?

Sara​—“Wewe Ni Mwanamke Mwenye Sura Nzuri”

Katika nchi ya Misri watumishi wa Farao waliona urembo wa Sara usio wa kawaida. Kilichotokea baada ya hapo huenda kikakushangaza.

Sara​—Mungu Alimwita “Binti ya Mfalme”

Kwa nini jina hilo jipya lilimfaa Sara?

Rebeka: “Mimi Niko Tayari Kwenda”

Zaidi ya kuwa na imani, Rebeka alionyesha sifa nyingine nyingi nzuri.

“Tafadhali Sikilizeni Ndoto Hii”

Familia yenye misukosuko ya Yakobo inatoa mafunzo muhimu kwa wale walio na familia za kambo leo.

“Ninawezaje Kufanya Ubaya Huu Mkubwa?”

Yosefu alishindaje jitihada za mke wa Potifa za kumshawishi?

“Je, Tafsiri Si za Mungu?”

Ni nini kilichomsaidia Yosefu afasiri kwa ujasiri ndoto ya mkuu wa wanyweshaji na mkuu wa waokaji, na hata ya Farao mwenyewe? Yosefu aliachaje kuishi gerezani na kuanza kuishi katika makao ya mfalme katika muda wa siku moja tu?

“Je, Mimi Niko Mahali pa Mungu?”

Ikiwa familia yenu haina amani kwa sababu ya wivu, usaliti, au chuki, simulizi la Biblia kuhusu Yosefu linaweza kukusaidia.

Ayubu—“Sitaukana Utimilifu Wangu!”

Simulizi la Biblia la Ayubu linaweza kutusaidiaje kukabiliana na hali ngumu, misiba, au majaribu mengine ya imani yetu?

Ayubu​—Yehova Alimponya Maumivu Yake

Tukimwiga Ayubu tutamkasirisha sana Shetani, hata hivyo, tutaufurahisha moyo wenye upendo wa Yehova!

Miriamu​—“Mwimbieni Yehova”!

Nabii wa kike Miriamu alichochewa kuwaongoza wanawake wa Israeli katika wimbo wa ushindi kwenye Bahari Nyekundu. Maisha yake yanatufundisha ujasiri, imani, na unyenyekevu.

Kuanzia Kutoka Hadi Mfalme wa Kwanza wa Israeli

Rahabu ‘Alitangazwa Kuwa Mwadilifu kwa Matendo’

Hadithi ya Rahabu inaonyesha kwamba Yehova anamwona kila mmoja wetu? Tunajifunza nini kutokana na imani yake?

‘Nilisimama kama Mama katika Israeli’

Simulizi la Biblia kuhusu Debora linatufundisha nini kuhusu imani na ujasiri?

Ruthu​—“Uendako Nitaenda”

Kwa nini Ruthu alikuwa tayari kuacha familia na nchi yake? Alisitawisha sifa gani ambazo zilimfanya awe mwenye thamani machoni pa Yehova?

Ruthu​—“Mwanamke Bora Sana”

Kwa nini ndoa kati ya Ruthu na Boazi ni muhimu sana? Tunaweza kujifunza nini kutoka kwa Ruthu na Naomi kuhusu familia?

Hana—Alimweleza Mungu Mahangaiko Yake

Imani ya Hana katika Yehova ilimsaidia kukabiliana na hali ngumu sana.

Samweli ‘Aliendelea Kukua Akiwa na Yehova’

Kwa nini maisha ya utotoni ya Samweli hayakuwa ya kawaida? Ni nini kilichomsaidia kusitawisha imani alipokuwa kwenye maskani?

Samweli—Alivumilia Licha ya Kuvunjwa Moyo

Sisi sote hukabili matatizo na mambo yanayovunja moyo ambayo hujaribu imani yetu. Uvumilivu wa Samweli unaweza kutufunza nini?

Kuanzia Mfalme wa Kwanza wa Israeli Hadi Kuzaliwa kwa Yesu

Yonathani​—“Hakuna Kitu Chochote Kinachoweza Kumzuia Yehova

Yonathani alishambulia kituo kizima cha ulinzi cha maadui waliojihami kwa silaha akiwa na mtumishi wake tu, na matokeo yanakumbukwa hadi leo.

“Vita Ni vya Yehova”

Ni nini kilichomwezesha Daudi kumshinda Goliathi? Tunaweza kujifunza nini kutoka na simulizi la Daudi?

Daudi na Yonathani​—“Wakashikamana na Kuwa Marafiki wa Karibu Sana”

Watu wawili waliokuwa na malezi na umri tofauti kabisa walikuwaje marafiki wa karibu sana? Simulizi lao linaweza kukusaidiaje kufanyiza urafiki leo?

Abigaili—Alitenda kwa Busara

Tunaweza kujifunza nini kutokana na ndoa ya Abigaili yenye matatizo?

Eliya—Alitetea ibada safi

Tunawezaje kumwiga Eliya tunaposhughulika na watu wanaopinga mafundisho ya Biblia?

Eliya—Alikaa Macho, na Kungoja

Nabii Eliya alionyeshaje kwamba alisali alipokuwa akisubiri Yehova atimize ahadi yake?

Eliya—Alifarijiwa na Mungu Wake

Ni nini kilichofanya Eliya avunjike moyo sana, hivi kwamba akatamani kufa?

Eliya Alivumilia Licha ya Ukosefu wa Haki

Je, umewahi kutendewa isivyo haki? Je, unatamani kuona Mungu akitekeleza haki? Soma jinsi unavyoweza kumwiga nabii mwaminifu Eliya.

Eliya​—Alivumilia Hadi Mwisho

Mfano wa Eliya wa uaminifu unaweza kutusaidia kuimarisha imani yetu tunapokabili hali ngumu.

Yona—Alijifunza Kutokana na Makosa Yake

Je, unaelewa ni kwa nini Yona alisita kukubali mgawo? Hadithi yake inatufundisha masomo muhimu kuhusu subira na rehema ya Yehova.

Yona—Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema

Simulizi la Yona linatusaidiaje kujichunguza kwa unyoofu?

Esta—Aliwatetea Watu wa Mungu

Ili kuonyesha upendo wa kujidhabihu kama wa Esta tunahitaji imani na ujasiri.

Esta—Alitenda kwa Hekima, Ujasiri na Bila Ubinafsi

Esta alitendaje bila ubinafsi kwa ajili ya Yehova na watu wake?

Kuanzia Kuzaliwa kwa Yesu Hadi Kifo cha Mitume

Maria​—“Tazama! Kijakazi wa Yehova!”

Jibu la Maria kwa malaika Gabrieli linafunua nini kuhusu imani yake? Alionyesha sifa gani nyingine muhimu?

Maria—Alikata “Kauli Moyoni Mwake”

Mambo ambayo Maria alijionea huko Bethlehemu yaliimarisha imani yake katika ahadi za Yehova.

Maria Alikabiliana na Upanga

Mfano wa Maria mama ya Yesu unaweza kukusaidia unapokabiliana na “upanga mrefu” wa majonzi.

Yosefu—Alikuwa Baba na Mume Aliyemwogopa Mungu

Yosefu aliilindaje familia yake? Kwa nini alimpeleka Maria na Yesu Misri?

Martha​—“Nimeamini”

Martha alionyeshaje imani thabiti hata wakati wa majonzi?

Maria Magdalene​—“Nimemwona Bwana!”

Mwanamke huyo mwaminifu alipewa pendeleo la kuwajulisha wengine habari hizo njema.

Petro—Alishinda Woga na Shaka

Shaka inaweza kuleta matokeo mabaya sana. Lakini Petro alishinda woga na shaka kuhusu kumfuata Yesu.

Petro—Alikuwa Mshikamanifu Licha ya Majaribu

Imani na ushikamanifu wa Petro ulimsaidiaje kukubali aliporekebishwa na Yesu?

Petro—Alijifunza Kusamehe Kutoka kwa Bwana Wake

Yesu alimfunzaje Petro kusamehe? Yesu alionyeshaje kwamba alikuwa amemsamehe Petro?

“Mtoto Wangu Mpendwa na Mwaminifu Katika Bwana”

Nini kilichomsaidia Timotheo aliyekuwa kijana mwenye haya kuwa mwangalizi Mkristo aliyefanikiwa sana?