Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ninyi ni wa maana.”​—MATAYO 10:31

Mungu Anakuona?

Mungu Anakuona?

MAMBO YENYE UUMBAJI UNATUFUNDISHA

Dakika 60 za kwanza zenye mutoto anafanya inje ya tumbo la uzazi ni wakati wa maana sana wa kufanya mabadiliko. Sababu gani? Kwa sababu wakati huo, mama wenye wanakuwa na uhusiano wa karibu na watoto wenye wametoka kuzaliwa, wanasaidia sana watoto wao wakomae muzuri. *

Ni nini inachochea mama ahangaikie kwa upendo mutoto wake mwenye ametoka kuzaliwa? Katika The Journal of Perinatal Education, Profesa Jeannette Crenshaw anafasiria kuwa kiasi kikubwa cha homoni yenye kuitwa oksitosini (ocytocine) “inachochea hisia za mama kisha tu kuzaa wakati anagusa mutoto wake, anamuangalia, na kumunyonyesha.” Homoni ingine yenye inatokezwa wakati huo “inasaidia mama kufanya uhusiano wa karibu na mutoto wake” na inasaidia uhusiano huo ukuwe nguvu. Sababu gani hilo ni jambo la maana?

Uhusiano wa karibu wenye mama anafanya pamoja na mutoto wake uliumbwa na Muumbaji wetu mwenye upendo, Yehova Mungu. * Mufalme Daudi alimutukuza Mungu kwa kumutosha “katika tumbo la uzazi” na kwa kumufanya ajisikie salama katika mikono ya mama yake. Alisali hivi: “Nimewekwa chini ya utunzaji wako tangu kuzaliwa kwangu; tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.”​—Zaburi 22:9, 10.

FIKIRIA JAMBO HILI: Ikiwa Mungu aliumba uwezo huo wa ajabu ili kuhakikisha kama mama atahangaikia mutoto wake kwa upendo na kutimiza mahitaji ya mutoto huyo, hauone kama ni jambo lenye kupatana na akili kuwa Mungu pia anapendezwa na kila mumoja wetu, sisi “watoto wa Mungu”?​—Matendo 17:29.

MAMBO BIBLIA INAFUNDISHA YANAONYESHA KAMA MUNGU ANATUHANGAIKIA KWA UPENDO

Yesu Kristo, mwenye anajua Muumbaji kuliko mutu mwengine yeyote, alifundisha hivi: “Ndege shomoro wawili wanauzishwa kwa feza moja ya kichele ya samani kidogo, haiko vile? Lakini hakuna hata mumoja wao mwenye ataanguka chini bila Baba yenu kujua. Lakini hata nywele zote za vichwa vyenu zimehesabiwa. Basi musiogope; ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.”​—Matayo 10:29-31.

Ni watu kidogo kati yetu ndio wanakazia uangalifu kila ndege mudogo mwenye tunaona, hata hivyo hakuna mwenye anaonaka wakati mumoja wao anaanguka kwenye udongo. Lakini Baba yetu wa mbinguni anaona kila mumoja wao! Na ndege​—hata ndege wengi​—hawako wa maana kwake kuliko mwanadamu. Kwa hiyo, somo liko wazi: Haupaswe ‘kuogopa’ na kuwaza kuwa Mungu hakuone. Tofauti na hilo, anapendezwa sana na wewe!

Mungu anapenda kabisa tukuwe na maisha ya muzuri na anatuhangaikia kwa upendo

Maandiko yanatuhakikishia

  • “Macho ya Yehova yako kila mahali, yakiangalia wabaya na wema.”​—MEZALI 15:3.

  • “Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.”​—ZABURI 34:15.

  • “Nitashangilia sana katika upendo wako mushikamanifu, kwa maana umeona mateso yangu; unajua taabu yangu nyingi.”​—ZABURI 31:7.

“NILIJISIKIA KUWA YEHOVA HAKUNIPENDA”

Kujua kwamba Mungu anapenda kabisa tukuwe na maisha ya muzuri na kwamba anatuhangaikia kwa upendo, kunaweza kubadilisha maisha yetu? Bila shaka jibu ni ndiyo, kama vile Hannah, * wa Inchi ya Uingereza, anaeleza:

“Mara nyingi sana, nilijisikia kuwa Yehova hakunipenda na kwamba hakuwa anajibia sala zangu. Niliwaza kuwa ni kwa sababu nilikosa imani. Nilifikiri kama nilikuwa ninapewa malipizi ao kusahauliwa kwa sababu sikuwa mutu wa maana. Nilijisikia kuwa Mungu hakunihangaikia.”

Hata hivyo, Hannah iko sasa hakika kuwa Yehova anamuhangaikia na kumupenda. Ni nini ilibadilisha mawazo yake? Anaeleza hivi: “Nilibadilika hatua kwa hatua. Ninakumbuka hotuba moja yenye kutegemea Biblia yenye ilitolewa kumepita miaka mingi. Hotuba hiyo kuhusu zabihu ya ukombozi ya Yesu ilinigusa sana moyo na ilinisaidia nikuwe hakika kama Yehova ananipenda. Na wakati sala zangu zinajibiwa, kila mara ninatokwa machozi juu nilitambua kuwa Yehova ananipenda. Pia, kwa kujifunza Biblia na kuenda kwenye mikutano ya Kikristo nimejifunza mambo mengi zaidi juu ya Yehova, sifa zake, na namna anatuhangaikia. Sasa ninaona waziwazi kuwa Yehova anatutegemeza na kutupenda sisi wote na kuwa iko na tamaa ya kusaidia kila mumoja wetu.”

Mambo yenye Hannah anasema yanatia moyo. Lakini namna gani unaweza kuwa hakika kama Mungu anakuelewa na kama anajua namna unajisikia? Habari yenye kufuata itajibia ulizo hilo.

^ fu. 3 Kwa mama fulani wenye wanashuka moyo kisha tu kuzaa, inaweza kuwa nguvu kufanya uhusiano wa karibu pamoja na watoto wao. Lakini, hawapaswe kufikiri kuwa ni kosa lao. Kulingana na Institut national de la santé mentale ya États-Unis, kushuka moyo kisha tu kuzaa “inaonekana kuwa kunatokana na matatizo ya kimwili na namna mutu anajisikia . . . lakini hakutokane na jambo fulani lenye mama anafanya ao hafanye.” Ili kupata maelezo zaidi juu ya habari hii, Ona habari “Kuelewa Mshuko wa Moyo Baada ya Kujifungua” katika Amuka! ya tarehe 8 Mwezi wa 6, 2003.

^ fu. 5 Yehova ni jina la Mungu kama vile imeonyeshwa katika Biblia.​—Zaburi 83:18.

^ fu. 15 Majina fulani katika habari hizi zenye kufuatana yamebadilishwa.