Ona video zinazopatikana

Namna Gani Kifo ya Yesu Ni Zabihu ya Ukombozi kwa Ajili ya Watu Wengi?

Namna Gani Kifo ya Yesu Ni Zabihu ya Ukombozi kwa Ajili ya Watu Wengi?

Jibu ya Biblia

 Zabihu ya Yesu ni njia yenye Mungu alitumia juu ya kukomboa wanadamu kutoka mu zambi na kifo. Biblia inaita damu yenye Yesu alimwanga kuwa bei ya ukombozi. (Waefeso 1:7; 1 Petro 1:18, 19) Njo maana Yesu alisema kama alikuya “kutoa uzima wake uwe ukombozi kwa watu wengi.”​—Matayo 20:28, La Sainte Bible en swahili de la R.D.Congo.

Juu ya nini kulikuwa lazima ya bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi?

 Adamu, mutu wa kwanza, alikuwa mukamilifu; ni kusema hakukuwa na zambi. Alikuwa na tumaini ya kuishi milele lakini alipoteza ile tumaini wakati alikosa kumutii Mungu. (Mwanzo 3:17-​19) Wakati alizala watoto, aliwapitishia zambi. (Waroma 5:12) Njo maana Biblia inasema kama Adamu ‘alijiuzisha’ na kuuzisha watoto wake katika utumwa wa zambi na kifo. (Waroma 7:14) Juu wazao wake wote hawakukuwa wakamilifu, hakuna mwenye angeweza kurudisha mambo yenye Adamu alipoteza.​—Zaburi 49:7, 8.

 Mungu alisikilia huruma wazao wa Adamu juu hawakukuwa na tumaini. (Yohana 3:16) Lakini juu Mungu anaheshimia kanuni zake za haki, hangeweza kuvuta zambi zao bila kuwa na musingi wenye kufaa. (Zaburi 89:14; Waroma 3:23-​26) Mungu anapenda wanadamu, njo maana aliweka musingi wenye ungewezesha zambi zao zisamehewe, na pia kuondolewa. (Waroma 5:6-8) Zabihu ya ukombozi njo ile musingi yenye Mungu aliweka.

Bei ya ukombozi inatia ndani mambo gani?

 Mu Biblia, maneno “bei ya ukombozi” inatia ndani mambo tatu yenye kufuata:

  1.   Ni malipo.​—Hesabu 3:46, 47.

  2.   Inakomboa.​—Kutoka 21:30.

  3.   Inalingana na samani ya kitu yenye ilipotezwa.

 Tuone namna bei ya ukombozi ya Yesu Kristo ilitimiza ile mambo tatu.

  1.   Ni malipo. Biblia inasema kama Wakristo ‘walinunuliwa kwa bei.’ (1 Wakorinto 6:20; 7:23) Ile bei ni damu ya Yesu yenye alimwanga juu ya ‘kununulia Mungu watu kutoka katika kila kabila na luga na watu na taifa.’​—Ufunuo 5:8, 9.

  2.   Inakomboa. Zabihu ya ukombozi ya Yesu inafanya watu ‘wakombolewe’ ao waachiliwe huru kutoka katika zambi.​—1 Wakorinto 1:30; Wakolosai 1:14; Waebrania 9:15.

  3.   Inalingana. Zabihu ya Yesu inalingana kabisa-kabisa na jambo yenye Adamu alipoteza, ni kusema, uzima mukamilifu. (1 Wakorinto 15:21, 22, 45, 46) Biblia inasema hivi: “Kama vile kupitia kukosa kutii kwa ule mutu mumoja [Adamu] wengi walifanywa kuwa watenda-zambi, vilevile pia kupitia kutii kwa mutu mumoja [Yesu Kristo] wengi watafanywa kuwa wenye haki.” (Waroma 5:19) Ile inatusaidia kuelewa namna kifo ya mutu mumoja inaweza kukomboa watenda-zambi wengi. Kwa kweli, zabihu ya Yesu ni “bei ya ukombozi yenye kulingana kwa ajili ya wote” wenye wanafanya mambo yenye inaombwa juu iwaletee faida.​—1 Timoteo 2:5, 6.