Zaburi 22:1-31

  • Kisha kupoteza tumaini anamusifu Mungu

    • “Mungu wangu, sababu gani umeniacha?” (1)

    • “Wanapigia nguo zangu kura” (18)

    • Kumusifu Mungu katika kutaniko (22, 25)

    • Dunia yote itamuabudu Mungu (27)

Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Paa Dike wa Mapambazuko.”* Muziki wa Daudi. 22  Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?+ Sababu gani uko mbali usiweze kuniokoa, Mbali na vilio vyangu vya uchungu?+   Mungu wangu, ninaendelea kuita wakati wa muchana, na wewe haunijibu;+ Na wakati wa usiku sinyamaze.   Lakini wewe ni mutakatifu,+ Umezungukwa na* sifa za Israeli.   Baba zetu walikutegemea wewe;+ Walitegemea, na ulikuwa unawaokoa.+   Walikulilia kwa sauti, na wakaokolewa; Walikutegemea, na hawakufanywa wapoteze tumaini.*+   Lakini mimi ni munyoo na siko mwanadamu, Ninachekwa* na wanadamu na kuzarauliwa na watu.+   Wale wote wenye wananiona wananichekelea;+ Wanazomea na kutikisa vichwa vyao kwa zarau:+   “Alijitia katika mikono ya Yehova. Acha Yeye amukomboe! Acha Yeye amuokoe, kwa sababu Yeye anamupenda sana!”+   Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi,+ Ni Wewe ulinifanya nijisikie salama kwenye maziwa ya mama yangu. 10  Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu kuzaliwa kwangu; Tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu, umekuwa Mungu wangu. 11  Usibakie mbali na mimi, kwa maana taabu iko karibu+ Na sina musaidizi mwingine.+ 12  Ngombe-dume wengi wadogo wananizunguka;+ Ngombe-dume wenye nguvu wa Bashani wananizunguka kwa ajili ya vita.+ 13  Wanafungua vinywa vyao wazi juu yangu,+ Kama simba mwenye kunguruma mwenye anapasua mawindo yake vipande-vipande.+ 14  Nimemwangwa kama maji; Mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu umekuwa kama nta;*+ Unayeyuka katika sehemu zangu za ndani kabisa.+ 15  Nguvu zangu zimekauka kama kipande cha chombo cha udongo;+ Ulimi wangu unashikamana na fizi* zangu;+ Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+ 16  Kwa maana imbwa wananizunguka;+ Wananizunguka kwa ajili ya vita kama kikundi cha watenda maovu,+ Kama vile simba, wako kwenye mikono yangu na miguu yangu.+ 17  Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+ Wananiangalia na kunikazia macho. 18  Wanagawana nguo zangu kati yao wenyewe, Na wanapigia nguo zangu kura.+ 19  Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+ Wewe ni nguvu zangu; kuja haraka unisaidie.+ 20  Uniokoe* kutokana na upanga, Uzima wangu wenye samani* kutokana na muguu wa* imbwa;+ 21  Uniokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ngombe-dume wa pori; Unijibu na uniokoe. 22  Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu;+ Katikati ya kutaniko nitakusifu.+ 23  Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu! Ninyi wote uzao wa* Yakobo, mumutukuze!+ Mumuogope sana, ninyi wote uzao wa* Israeli. 24  Kwa maana hajazarau wala kuchukizwa na mateso ya ule mwenye kukandamizwa;+ Hajamuficha uso wake.+ Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+ 25  Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+ Nitatimiza naziri zangu mbele ya wale wenye kumuogopa. 26  Wapole watakula na kushiba;+ Wale wenye kumutafuta Yehova watamusifu.+ Mufurahie maisha* milele. 27  Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumuendea Yehova. Familia zote za mataifa zitainama mbele yako.+ 28  Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+ Anatawala juu ya mataifa. 29  Watu wote wenye kufanikiwa* katika dunia watakula na kumuinamia; Wale wote wenye kushuka katika mavumbi watapiga magoti mbele yake; Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza kulinda uzima wao.* 30  Wazao wao watamutumikia;* Kizazi chenye kitakuja kitaambiwa kuhusu Yehova. 31  Watakuja na kusimulia kuhusu haki yake. Wataambia watu wenye bado hawajazaliwa mambo yenye amefanya.

Maelezo ya Chini

Pengine ni sauti ao mutindo wa muziki.
Ao “Umekaa ukiwa mufalme kati ya (juu ya).”
Ao “hawakupatishwa haya.”
Ao “Ninalaumiwa.”
Tnn., “Nimetupwa kwako.”
Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
Fizi ni nyama zenye kushikilia meno katika kinywa.
Ao “Uokoe nafsi yangu.”
Tnn., “Kitu changu cha pekee,” ni kusema, nafsi yake, ao uzima wake.
Tnn., “mukono wa.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Moyo wenu uishi.”
Tnn., “wanene.”
Ao “nafsi zao.”
Tnn., “Mbegu yao itamutumikia.”