Ona video zinazopatikana

Funzo la Biblia Ni Nini?

Funzo la Biblia Ni Nini?

Mashahidi wa Yehova wanatolea watu programu ya kujifunza nao Biblia inayojibu maulizo mengi, kama vile:

  • Mungu Ni Nani?

  • Je, Mungu ananihangaikia?

  • Namna gani naweza kuwa na maisha mazuri ya ndoa?

  • Namna gani naweza kupata furaha katika maisha?

Hapa chini utapata majibu ya maulizo mengi juu ya programu yetu ya kujifunza Biblia.

Funzo linaendeshwa namna gani? Tunachukua habari kama vile “Mungu” ao “ndoa” na tunachunguza maandiko mbalimbali ya Biblia yanayozungumuzia habari hiyo. Kwa kufanya hivyo tunajua mawazo ya Biblia juu ya habari hizo, na hivyo tunaacha Biblia yenyewe itoe majibu.

Kitabu tunachotumia ili kujifunza Biblia ni Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kitabu hiki kinaonyesha waziwazi yale ambayo Biblia inasema juu ya Mungu, Yesu, na wakati wetu ujao.

Funzo la Biblia linalipishwa ngapi? Funzo linafanywa bila malipo, na hatuuzishe vitabu tunavyotumia ili kujifunza.

Funzo linachukua saa ngapi? Watu wengi wanajiwekea saa moja ao zaidi kila juma ili kujifunza Biblia pamoja nasi. Lakini hilo linategemea hali ya mutu anayejifunza. Tunaheshimu programu ya mwanafunzi.

Itakuwa namna gani ninapoomba funzo la Biblia? Unapoomba funzo la Biblia, Shahidi wa Yehova atakutembelea saa na mahali panapokufaa. Atachukua wakati kidogo ili kukuonyesha namna funzo linavyoendeshwa. Ukipendezwa na funzo unaweza kuendelea kujifunza.

Nikikubali Funzo la Biblia, je, ninapaswa kuwa Shahidi wa Yehova? Hapana. Mashahidi wa Yehova wanapenda kufundisha watu juu ya Biblia, lakini hatulazimishe mutu awe Shahidi wa Yehova. Lakini tunamuonyesha yale ambayo Biblia inasema, tukijua kama kila mutu iko na haki ya kuchagua mambo ambayo ataamini.—1 Petro 3:15.