Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUNARA WA MULINZI Na. 3 2018 | Mungu Anakuhangaikia?

MUNGU ANAKUHANGAIKIA?

Wakati musiba unatokea ao wakati watu wanateseka na kufa, tunaweza kujiuliza ikiwa Mungu anaona ao ikiwa anahangaikia jambo hilo. Biblia inasema hivi:

“Kwa maana macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza sala yao ya kumulilia Mungu, lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya.”​—1 Petro 3:12.

Gazeti hili la Munara wa Mulinzi linaonyesha namna Mungu anatusaidia na jambo lenye iko anafanya ili kuondoa mateso yote.

 

“Mungu Alikuwa Wapi?”

Hali fulani yenye kuogopesha imekufanya ujiulize ikiwa Mungu anakuhangaikia kipekee?

Mungu Anakuona?

Ni mambo gani yanakuhakikishia kama Mungu anapenda kabisa ukuwe na maisha ya muzuri?

Mungu Anakuelewa?

Uwezo wa pekee wa Mungu wa kutujua na kujua chembe zetu za uriti unatuhakikishia kuwa anatuelewa kabisa hata katika mambo madogo-madogo.

Mungu Iko na Huruma?

Biblia inatuhakikishia kuwa Mungu anatuona, anatuelewa, na kuwa anatusikilia huruma.

Mateso​​—Ni Malipizi Kutoka kwa Mungu?

Mungu anatumia magonjwa ao misiba ili kupatia watu malipizi kwa sababu ya zambi zao?

Ni Nani Anatuletea Mateso?

Biblia inafunua sababu tatu kubwa zenye zinafanya watu wateseke.

Hivi Karibuni, Mungu Atamaliza Mateso Yote

Ni nini inatuhakikishia kama Mungu atamaliza mateso yote na ukosefu wa haki?

Kujua Kama Mungu Anakuhangaikia Kutakuletea Faida Gani?

Maandiko yanatusaidia tukuwe na imani katika ahadi za Mungu kwa ajili zaidi.

Mungu Anajisikia Namna Gani Juu ya Mateso Yako?

Maandiko haya yanaweza kukusaidia kuelewa namna Mungu anajisikia wakati watu wanateseka.