Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ufalme wa Mungu utakapokuwa ukitawala, watu “watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”​—Zaburi 37:11

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na mahangaiko?

Una maoni gani?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

Biblia inasema hivi

“[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake [Mungu], kwa sababu yeye anawajali ninyi.” (1 Petro 5:⁠7) Biblia inatoa uhakikisho wa kwamba Mungu anaweza kukusaidia kupunguza mahangaiko uliyo nayo.

Mambo mengine tunayojifunza katika Biblia

  • Kupitia sala, unaweza kupata “amani ya Mungu” ambayo hupunguza mahangaiko.​—Wafilipi 4:​6, 7.

  • Kwa kuongezea, kusoma Neno la Mungu kunaweza kukusaidia ukabiliane na mkazo.​—Mathayo 11:​28-​30.

Je, mahangaiko yatakwisha?

Baadhi ya watu wanaamini . . . kwamba mahangaiko na mkazo ni sehemu ya maisha ya wanadamu, na wengine huamini kwamba mahangaiko huisha pale tu mtu anapokufa. Wewe una maoni gani?

Biblia inasema hivi

Mungu ataondoa mambo yanayosababisha mahangaiko. “Kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:4.

Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?