Hamia kwenye habari

Kwa Nini Watu Hufa?

Kwa Nini Watu Hufa?

Jibu la Biblia

 Ni jambo la kawaida kujiuliza kwa nini watu hufa, hasa mpendwa wetu wa karibu anapokufa. Biblia inasema: “Mchomo unaotokeza kifo ni dhambi.”​—1 Wakorintho 15:56.

Kwa nini watu wote wanatenda dhambi na kufa?

 Wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa, walipoteza uhai wao kwa sababu walitenda dhambi. (Mwanzo 3:17-19) Kifo kilikuwa matokeo ya uasi wao dhidi ya Mungu, kwa sababu yeye ndiye “chemchemi ya uzima.”​—Zaburi 36:9; Mwanzo 2:17.

  Adamu alipitisha matokeo ya dhambi kwa wazao wake wote. Biblia inasema: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Waroma 5:12) Wanadamu wote hufa kwa sababu wote wanatenda dhambi.​—Waroma 3:23.

Jinsi kifo kitakavyoondolewa

 Mungu anaahidi wakati ambapo “atameza kifo milele.” (Isaya 25:8) Ili kumaliza kifo, lazima aondoe dhambi, chanzo cha kifo. Mungu atatimiza hayo kupitia Yesu Kristo, “ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.”​—Yohana 1:29; 1 Yohana 1:7.