Hamia kwenye habari

Ni Nani Wanaoenda Kuzimu?

Ni Nani Wanaoenda Kuzimu?

Jibu la Biblia

 Kuzimu (“Sheoli” na “Hadesi” katika lugha za awali za Biblia) ni kaburi, na si mahali pa moto wa mateso. Ni nani wanaoenda kuzimu? Ni watu wote, wawe wema au wabaya. (Ayubu 14:13; Zaburi 9:​17) Biblia inataja kwamba kaburi hilo la ujumla la wanadamu ni “nyumba ya kukutania ya kila mtu aliye hai.”​—Ayubu 30:23.

 Yesu mwenyewe alipokufa alienda kuzimu. Hata hivyo, ‘hakuachwa kuzimu,’ kwa sababu Mungu alimfufua.​—Matendo 2:​31, 32, Habari Njema kwa Watu Wote.

Je Watu Watabaki Kuzimu Milele?

 Kwa nguvu za Mungu, Yesu atawarudisha kwenye uhai wale wote walio kuzimu. (Yohana 5:​28, 29; Matendo 24:15) Unabii unaopatikana katika Ufunuo 20:13 unasema hivi kuhusu ufufuo wa wakati ujao: “Kifo na kuzimu vikawatoa nje wafu waliokuwa ndani yao.” (Biblia Habari Njema) Baada ya watu kufufuliwa, hakuna mtu ambaye atarudi huko tena kwa sababu “kifo hakitakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:​3, 4; 20:14.

 Si kila mtu anayekufa huenda kuzimu. Biblia inaonyesha kwamba kuna wale ambao wamezoea sana kutenda dhambi hivi kwamba hawataki kubadilika. (Waebrania 10:26, 27) Watu hao wanapokufa, hawaendi kuzimu, bali wanaenda Gehena, ambayo inafananisha uharibifu wa milele. (Mathayo 5:29, 30) Kwa mfano, Yesu alisema kwamba baadhi ya viongozi wa kidini wanafiki katika siku zake wangeenda Gehena.​—Mathayo 23:27-​33.