Ayubu 14:1-22

  • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

    • Maisha ya mwanadamu ni mafupi na yamejaa taabu (1)

    • “Hata mti una tumaini” (7)

    • “Laiti ungenificha Kaburini!” (13)

    • “Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?” (14)

    • Mungu ataitamani sana kazi ya mikono yake (15)

14  “Mwanadamu anayezaliwa na mwanamke,Maisha yake ni mafupi+ na yamejaa taabu.*+   Huchanua kama ua na kisha hunyauka;*+ Hukimbia kama kivuli na kutoweka.+   Naam, umemkazia jicho lako,Nawe unamleta* mbele zako katika hukumu.+   Ni nani anayeweza kutokeza mtu safi kutokana na mtu asiye safi?+ Hakuna awezaye!   Ikiwa siku zake zinajulikana,Basi unajua idadi ya miezi yake;Umemwekea mpaka ambao hawezi kuvuka.+   Yageuzie mbali macho yako ili apumzike,Mpaka atakapomaliza siku yake, kama kibarua.+   Kwa maana hata mti una tumaini. Ukikatwa, utachipuka tena,Na matawi yake yataendelea kukua.   Mizizi yake ikizeekea ardhiniNa kisiki chake kikifia udongoni,   Utachipuka unaponusa maji;Nao utatokeza matawi kama mmea mpya. 10  Lakini mwanadamu hufa na kulala bila uwezo wowote;Mwanadamu anapokufa, yuko wapi?+ 11  Maji hutoweka baharini,Na maji ya mto hupungua na kukauka. 12  Mwanadamu pia hulala naye haamki.+ Mpaka mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka,Wala hawataamshwa kutoka katika usingizi wao.+ 13  Laiti ungenificha Kaburini,*+Ungenificha mpaka hasira yako ipite,Laiti ungenipimia wakati hususa na kunikumbuka!+ 14  Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?+ Nitangojea sikuzote za utumishi wangu wa kulazimishwaMpaka kitulizo changu kitakapokuja.+ 15  Utaita, nami nitakujibu.+ Utaitamani sana* kazi ya mikono yako. 16  Lakini sasa, unaendelea kuhesabu kila hatua yangu;Unatafuta tu dhambi zangu. 17  Kosa langu limefungiwa katika mfuko,Nawe unaufunga uovu wangu kwa gundi. 18  Kama mlima unavyoanguka na kuporomokaNa mwamba unavyong’oka mahali pake, 19  Kama maji yanavyomomonyoa mawe Na mafuriko yanavyosomba udongo,Ndivyo ulivyoharibu tumaini la mwanadamu anayeweza kufa. 20  Unaendelea kumshinda nguvu mpaka anapoangamia;+Unaibadili sura yake, na kumfukuza. 21  Wanawe wanaheshimiwa, lakini yeye hajui;Wanadharauliwa, lakini yeye hatambui.+ 22  Huhisi maumivu anapokuwa tu angali hai;Yeye* huomboleza wakati tu angali anaishi.”

Maelezo ya Chini

Au “msukosuko.”
Au labda, “hukatwa.”
Tnn., “unanileta.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Utakuwa na hamu kubwa kwa ajili ya.”
Au “Nafsi yake.”