Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Niko na Roho Nguvu?

Niko na Roho Nguvu?

 Uko na roho nguvu? Ulishaka . . .

  •   kufiwa na mupendwa?

  •   kupambana na ugonjwa wenye kuendelea?

  •   kupigwa na musiba wa asili?

 Habari fulani zinaonyesha kama haiko tu magumu ya nguvu njo inaombaka kuwa na roho nguvu. Hata mahangaiko ya kila siku inaweza kukutesa. Njo maana ni jambo ya maana sana kuwa na roho nguvu, ukuwe na magumu ya kidogo ao ya nguvu.

 Kuwa na roho nguvu maana yake nini?

 Kuwa na roho nguvu, ni kuwa na uwezo wa kushugulikia magumu na kuendelea kuwa nguvu. Watu wenye kuwa na roho nguvu, nao pia wanapataka magumu sawa vile watu wote. Lakini wanaishinda, wanaendelea kuwa na mawazo ya muzuri na kuwa tena nguvu kuliko vile walikuwa wakati walikuwa wanapambana na ile magumu.

Vile tu miti fulani inakunjamaka wakati wa upepo mukali lakini inasimama tena kisha ile upepo kupita, ni vile unaweza kujisikia muzuri kisha kupita mu magumu ya nguvu

 Juu ya nini uko na lazima ya kuwa na roho nguvu?

  •   Juu kila mutu anapataka magumu. Biblia inasema: “Haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, . . . wala haiko wenye ujuzi ndio wanafanikiwa kila mara, kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.” (Muhubiri 9:11) Ile andiko inapenda kutufundisha nini? Hata watu wazuri wanatesekaka​—na mara mingi haiko juu walifanya jambo ya mubaya.

  •   Juu kuwa na roho nguvu kunatulinda. Mushauri mumoja wa masomo ya segondere anasema kama hii masiku, wanafunzi wengi wako wanakuja ku biro yake na walisha kasirika na wanashindwa kujizuia juu tu walipata alama za chini, ao juu watu fulani waliandika mambo ya mubaya juu yao ku site za kupashana habari na watu wengi. Anasema tena kama, ile matatizo inaonekana kuwa kidogo. Lakini ikiwa mwanafunzi hajue namna ya kuimaliza kwa njia ya muzuri, akili yake inaweza kuvurugika. *

  •   Juu kuwa na roho nguvu kutakusaidia leo na wakati utakomala. Dr. Richard Lerner aliandika hivi juu ya mambo yenye kuvunja moyo: “Kati ya mambo yenye inaonyesha kama mutu anakomala, kuko kujua kuvumilia wakati anapambana na mambo yenye kuvunja moyo, kujiwekea miradi ya mupya ao kujaribu njia zingine za kumusaidia afikie miradi yake.” *

 Namna gani unaweza kupata roho nguvu?

  •   Jua ukubwa wa magumu yako. Ujue kutofautisha magumu ya kidogo na ya munene. Biblia inasema: “Mupumbavu anaonyesha pale pale kwamba ameuzika, lakini mutu mwerevu anapuuza matusi.” (Mezali 12:16) Haiko kila magumu njo inapaswa kukusumbua sana.

     “Ku masomo, wanafunzi wenzangu walikuwa wanalalamika-lalamika juu ya mambo yenye haiko hata ya kulalamikia. Kisha sasa marafiki wao wanatumia site za kupashana habari na watu wengi juu ya kuwaambia kama ni vile njo walipaswa kufanya​—Na ile inafanya walalamike tena zaidi. Kufanya vile hakuwasaidie wajue namna ya kumaliza magumu yao.”​—Joanne.

  •   Ujifunze kupitia wengine. Mezali moja ya Biblia inasema hivi: “Kama vile chuma kinanoa chuma, ni vile pia mutu ananoa rafiki yake.” (Mezali 27:17) Tunaweza kujifunza mambo ya lazima sana kwa watu wenye walishakapita mu magumu ya nguvu sana.

     “Wakati unazungumuza na wengine, utaona kama walipataka majaribu ya nguvu sana, na sasa wako sawa. Zungumuza nao na ujue mambo yenye walifanya na yenye hawakufanya juu ya kupambana na ile majaribu.”​—Julia.

  •   Ukuwe muvumilivu. Biblia inasema: “Mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena.” (Mezali 24:16) Inakamata wakati juu ya kuitikia mambo yenye ilitupata, kwa hiyo usishangae kama wakati fulani unahuzunika. Jambo ya lazima ni ‘kusimama tena.’

     “Wakati unatoka mu magumu ya nguvu, inaomba akili na moyo wako vitulie. Ile haifanyike mara moja. Vile njo mambo inakuwaka na inakamataka wakati. Nimeelewa kama vile wakati iko inapita na njo vile inakuwa mwepesi kujisikia muzuri tena.”​—Andrea.

  •   Ukuwe mwenye shukrani. Biblia inasema: “Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.” (Wakolosai 3:15) Hata kama uko na magumu ya namna gani, hauwezi kukosa mambo ya kukuchochea uonyeshe shukrani. Fikiria mambo tatu yenye inakusaidia uendelee kufurahia maisha hata kama uko na magumu.

     “Wakati uko na magumu, ni mwepesi kujiuliza, ‘juu ya nini hii mambo iko inanifikia tu miye?’ Jambo yenye itakusaidia ukuwe na roho nguvu haiko kuwaza sana juu ya magumu yako, lakini ni kuwaza sana juu ya mambo ya muzuri mu maisha yako, na kuwa mwenye shukrani juu ya mambo yenye uko nayo ao juu ya mambo yenye unaweza kufanya.”​—Samantha.

  •   Ukuwe mwenye kutosheka. Mutume Paulo alisema: “Nimejifunza kutosheka hata hali zangu zikuwe namna gani.” (Wafilipi 4:11) Paulo hakukuwa na uwezo wa kubadilisha magumu yenye ilimupata. Lakini alikuwa na uwezo wa kubadilisha namna yake ya kutenda wakati alikuwa na ile magumu. Paulo aliazimia kuwa mwenye kutosheka.

     “Jambo yenye nilijifunza juu yangu mwenyewe ni kwamba namna nilikuwa natenda wakati wa magumu haikukuwa muzuri kabisa. Sasa, muradi yangu ni kuwa na maoni ya muzuri hata nipatwe na hali ya namna gani. Ile itaniletea miye mwenyewe faida na wale wenye kuwa pembeni yangu.”​—Matthew.

  •   Usali. Biblia inasema: “Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.” (Zaburi 55:22) Sala haiko jambo yenye unafanya juu tu ujisikie muzuri. Ni kuzungumuza na Muumbaji wako mwenye ‘anakuhangaikia.’​—1 Petro 5:7.

     “Sipaswe kupiganisha magumu yangu miye peke. Wakati ninamuambia Mungu mambo yangu waziwazi bila kumuficha kitu, na wakati ninamushukuru kisha kuona namna ananibariki, mawazo yangu ya mubaya inakimbia juu nakaza akili yangu juu ya baraka za Yehova. Kusali ni jambo ya lazima sana!”​—Carlos.

^ Mu kitabu Disconnected, ya Thomas Kersting.

^ Mu kitabu The Good Teen—Rescuing Adolescence From the Myths of the Storm and Stress Years.