Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Namna gani Ninaweza Kuzoeza Zamiri Yangu?

Namna gani Ninaweza Kuzoeza Zamiri Yangu?

 Zamiri yako inaweza kufananishwa na nini kati ya vitu vyenye kutajwa hapa chini?

  •   boussole

  •   kioo

  •   rafiki

  •   muamuzi

 Zamiri inaweza kufananishwa na ile mambo yote ine. Tuone juu ya nini.

 Zamiri ni nini?

 Zamiri yako ni sauti yako ya ndani yenye inakusaidia kujua kama jambo fulani ni la muzuri ao la mubaya. Biblia inasema kama zamiri iko sawa vile “sheria iliyoandikwa katika mioyo” ya wanadamu. (Waroma 2:15, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Zamiri ya muzuri inakusaidia uchunguze uamuzi wenye unapenda kukamata ao wenye ulishakamata.

  •   Zamiri yako iko kama boussole. Inakuonyesha njia ya muzuri kusudi uepuke hatari.

  •   Zamiri yako iko kama kioo. Inakuonyesha kanuni zenye zinapaswa kukuongoza mu maisha na inakuonyesha namna uko kwa ndani.

  •   Zamiri yako iko kama rafiki muzuri. Kama unaisikiliza, inaweza kukupatia mashauri ya muzuri na kukusaidia upate matokeo ya muzuri mu mambo yenye unafanya.

  •   Zamiri yako iko kama muamuzi. Inakuhukumu wakati unafanya kosa.

Zamiri ya muzuri inaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri

 Wazo kubwa: Zamiri yako ni kitu ya maana yenye inaweza kukusaidia (1) ukamate maamuzi ya muzuri na (2) uhuzunikie makosa yako na uone namna ya kuiacha.

 Juu ya nini unapaswa kuzoeza zamiri yako?

 Biblia inatuambia ‘tuendelee kuwa na zamiri ya muzuri.’ (1 Petro 3:16) Ni nguvu kufanya vile kama hatuzoeze zamiri yetu.

 “Nilizoea kudanganya wazazi wangu kuhusu fasi kwenye nilikuwa na nilikuwa ninawaficha wasijue fasi kwenye nilikuwa. Ku mwanzo, zamiri yangu ilinisumbua, lakini kisha wakati fulani nilianza kuona kama kufanya vile ni kawaida tu.”—Jennifer.

 Kisha, zamiri ya Jennifer ilimuchochea aambie wazazi wake kama alikuwa anawadanganya na ilimuchochea aache kufanya vile.

 Fikiria jambo hili: Ni wakati gani njo zamiri ya Jennifer ilipaswa kumuonya?

 “Kuishi maisha ya unafiki kunaletaka matatizo na mahangaiko. Kama tu zamiri yako inakuruhusu kukamata uamuzi moja mubaya, inakuwa mwepesi zaidi kwako kukamata uamuzi mwingine mubaya.”—Matthew.

 Watu fulani hawasikilizake hata kidogo zamiri yao. Biblia inasema kama ‘wameishiwa na ufahamu wote wa mambo yenye kuwa sawa.’ (Waefeso 4:19) Tafsiri Habari Njema kwa Watu Wote inatafsiri ile maneno hivi: “Wamepotoka na hawana aibu [ao haya].”

 Fikiria jambo hili: Watu wenye zamiri yao haiwasumbuake wakati wanafanya makosa, unawaza wao njo wako na maisha ya muzuri? Ni magumu gani yenye hawawezi kuepuka?

 Wazo kubwa: Ili uendelee kuwa na zamiri ya muzuri, unapaswa kuzoeza nguvu zako za ufahamu ili ziweze kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.—Waebrania 5:14.

 Namna gani unaweza kuzoeza zamiri yako?

 Ili kuzoeza zamiri yako, uko na lazima ya kanuni za kukuongoza. Wamoja wanafuata kanuni zenye zimewekwa na:

  •   familia na desturi za kwao

  •   watu wa miaka yao

  •   wachezaji na wapiga-muziki wenye kujulikana sana

 Lakini, kanuni za Biblia zenye zinaonyesha namna tunapaswa kuishi njo za muzuri zaidi. Ile haishangaze, kwa sababu Biblia ‘iliongozwa na roho ya Mungu.’ Yeye njo alituumba na yeye njo anajua mambo yenye inaweza kutuletea faida.—2 Timoteo 3:16.

 Fikiria kanuni fulani za Biblia.

 KANUNI: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”—Waebrania 13:18.

  •   Namna gani ile kanuni inaweza kusaidia zamiri yako kama unashawishiwa kuiba majibu wakati wa mashindano ku masomo, kuiba vitu, ao kudanganya wazazi wako?

  •   Kama zamiri yako inakuchochea ukuwe munyoofu mu mambo yote, unawaza ile itakusaidia namna gani sasa na wakati wenye kuja?

 KANUNI: “Mukimbie uasherati.”—1 Wakorinto 6:18.

  •    Namna gani ile kanuni inaweza kusaidia zamiri yako kama unashawishiwa kuangalia pornografia ao kufanya ngono na haujaoa ao kuolewa?

  •   Kama zamiri yako inakuchochea ukimbie uasherati, unawaza ile itakusaidia namna gani sasa na wakati wenye kuja?

 KANUNI: “Mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyingi, na musameheane kwa kupenda.”—Waefeso 4:32.

  •    Namna gani ile kanuni inaweza kukusaidia wakati hausikilizane na ndugu yako, dada yako, ao rafiki yako?

  •   Kama zamiri yako inakuchochea ukuwe na huruma na ukuwe mwenye kusamehe, unawaza ile itakusaidia namna gani sasa na wakati wenye kuja?

 KANUNI: “Yehova . . . anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.”—Zaburi 11:5.

  •    Namna gani ile kanuni inaweza kukusaidia wakati unachagua filme, programu za televizyo, na michezo ya video?

  •   Kama zamiri yako inakuchochea ukatae mambo ya kujifurahisha yenye kuonyesha jeuri, unawaza ile itakusaidia namna gani sasa na wakati wenye kuja?

 HADISI YA KWELI: “Niko na marafiki wenye walikuwa wanacheza michezo ya video yenye kuonyesha jeuri na miye nilikuwa nacheza ile michezo. Kisha baba yangu alinikataza kuicheza. Kwa hiyo, nilianza kucheza ile michezo wakati tu nilikuwa ninatembelea marafiki wangu. Wakati nilikuwa narudia ku nyumba sikukuwa naambia wazazi wangu kitu. Wakati baba yangu alikuwa ananiuliza kama kuko kitu kinanisumbua, nilikuwa ninasema kama niko sawa. Lakini siku moja nilisoma Zaburi 11:5 na nikaanza kujisikia mubaya kwa sababu ya mambo yenye nilikuwa ninafanya. Nilielewa kama iliomba niache kucheza ile michezo ya video. Mara hiyo, nilifanya vile. Mufano wangu ulichochea marafiki wangu pia waache kucheza michezo ya video yenye kuonyesha jeuri.”—Jeremy.

 Fikiria jambo hili: Ni wakati gani zamiri ya Jeremy ilianza kumusumbua, na ni wakati gani alianza kuisikiliza? Hadisi ya Jeremy inakufundisha nini?

 Wazo kubwa: Zamiri yako inaonyesha kama uko mutu wa namna gani na ni mambo gani njo unaona kuwa ya maana. Sasa wewe kipekee, zamiri yako inaonyesha kama uko mutu wa namna gani?