Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ngono ya Kinywa, Nayo Ni Ngono?

Ngono ya Kinywa, Nayo Ni Ngono?

 Kulingana na ripoti ya shirika fulani ya Amerika ya kushugulikia magonjwa (Centers for Disease Control and Prevention), karibu nusu ya vijana wa kati ya miaka 15 na 19 wenye waliulizwa walisema kama walishakafanya ngono ya kinywa. Sharlene Azam, mwandikaji wa kitabu Oral Sex Is the New Goodnight Kiss, anasema hivi: “Ukiongea na vijana kuhusu ngono ya kinywa, watakuambia kama haiko kosa. Kwa kweli hawaione kuwa ngono.

 Unawaza nini?

 Jibia ndiyo ao hapana ku maulizo yenye kufuata.

  1.   Kijana mwanamuke anaweza kupata mimba kama anafanya ngono ya kinywa?

    1.   Ndiyo

    2.   Hapana

  2.   Ngono ya kinywa iko na hatari yoyote ku afya?

    1.   Ndiyo

    2.   Hapana

  3.   Ngono ya kinywa nayo ni ngono?

    1.   Ndiyo

    2.   Hapana

 Mambo iko namna gani kabisa?

 Linganisha majibu yako na majibu yenye kufuata

  1.   Kijana mwanamuke anaweza kupata mimba kama anafanya ngono ya kinywa?

     Jibu: Hapana. Na njo maana watu wengi wanajidanganyaka kwa kuwaza kama ngono ya kinywa haina hatari yoyote.

  2.   Ngono ya kinywa iko na hatari yoyote ku afya?

     Jibu: Ndiyo. Mutu mwenye kufanya ngono ya kinywa anaweza kupata magojwa saa vile hépatite A ao B, upele ku viungo vya uzazi, blennorragie, vidonda ku viungo vya uzazi, SIDA, na syphilis.

  3.   Ngono ya kinywa nayo ni ngono?

     Jibu: Ndiyo. Matendo yoyote yenye kuhusisha viungo vya uzazi vya mutu mwingine, sawa vile ngono kati ya mwanaume na mwanamuke, ngono ya kinywa, ngono ya mukundu, na kugusa-gusa viungo vya uzazi vya mutu mwingine, ile yote ni ngono.

 Juu ya nini ni muzuri kufikiria hii jambo?

 Ona maandiko fulani ya Biblia yenye inahusu ngono ya kinywa.

 Biblia inasema: “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba munapaswa . . kujiepusha na uasherati.”​—1 Watesalonike 4:3.

 Neno ya kwanza-kwanza yenye inatafsiriwa uasherati inamaanisha aina yote ya matendo ya ngono kati ya watu wenye hawayaoana, ngono kati ya mwanaume na mwanamuke, ngono ya kinywa, ngono ya mukundu, na kugusa-gusa viungo vya uzazi vya mutu mwingine. Mutu mwenye kufanya uasherati anaweza kupata matatizo ya mingi sana. Na ya nguvu sana mu zote ni kuharibu urafiki wake pamoya na Mungu.​—1 Petro 3:12.

 Biblia inasema: “Mutu yeyote mwenye kuwa na mazoea ya kufanya uasherati anatendea mwili wake mwenyewe zambi.”​—1 Wakorinto 6:18.

 Ngono ya kinywa inaweza kuletea mutu matatizo ya afya, inaweza kuharibu urafiki wa mutu pamoya na Mungu, na inaweza hata kuletea mutu huzuni. Kitabu Talking Sex With Your Kids kinasema hivi: “Haiko kufanya ngono kwa njia ya kawaida tu njo kunaweza kufanya mutu ajisikie kuwa ametumiwa, akuwe na huzuni, ao ajisikie kuwa hana mutu wa kumulinda. Hisia zote za mubaya zenye mutu anaweza kusikia kisha kufanya ngono mu hali zenye hazifae, anaweza kusikia kisha kufanya aina yoyote ya ngono. Ngono ni ngono.”

 Biblia inasema: “Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida.”​—Isaya 48:17.

 Unaamini kuwa sheria za Mungu juu ya ngono zinaweza kukuletea faida? Ao unawaza kama zinakufunga? Juu ya kupata jibu ya ile maulizo, fikiria barabara yenye kuwa na magari ya mingi na yenye kuwa na alama za mingi za barabara. Unawaza zile alama zinakufunga ao zinakulinda? Unawaza nini itatokea kama weye ao watu wengine hawaziheshimie?

Sheria za barabara zinakuzuia kufanya mambo yenye unapenda lakini zinakulinda. Vilevile, sheria za Mungu zinakuzuia kufanya mambo fulani, lakini zinakulinda

 Ni vile pia kuhusu kanuni za Mungu. Kama unakatala kuzifuata, utavuna kile unapanda. (Wagalatia 6:7) Kitabu Sex Smart inasema kama “wakati unaacha mambo yenye unaamini na unaanza kufanya mambo yenye unaona kuwa haiko sawa, hautajiheshimia tena.” Lakini kama unafuata kanuni za Mungu, utakuwa na mwenendo muzuri. Na zaidi ya yote utaendelea kuwa na zamiri safi.​—1 Petro 3:16.