Kwa Wafilipi 4:1-23

  • Umoja, kufurahi, mawazo yenye kufaa (1-9)

    • Musihangaike juu ya jambo lolote (6, 7)

  • Shukrani kwa zawadi za Wafilipi (10-20)

  • Salamu za mwisho (21-23)

4  Kwa hiyo, ndugu zangu wenye ninapenda na ninatamani kuwaona, furaha yangu na taji langu,+ musimame imara+ katika njia hii katika Bwana, wapendwa wangu.  Ninamutia moyo Euodia na ninamutia moyo Sintike wakuwe na akili moja katika Bwana.+  Ndiyo, ninakuomba wewe pia, ukiwa mufanyakazi mwenzangu wa kweli,* uendelee kusaidia wanamuke hao wenye wamekazana* bega kwa bega pamoja na mimi kwa ajili ya habari njema, pamoja na Klementi na vilevile wale wafanyakazi wenzangu wengine, wenye majina yao yako katika kitabu cha uzima.+  Mufurahi sikuzote katika Bwana. Nitasema tena, Mufurahi!+  Usawaziko wenu+ ujulikane kwa watu wote. Bwana iko* karibu.  Musihangaike juu ya jambo lolote,+ lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu* pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu;+  na amani+ ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu+ na nguvu zenu za akili* kupitia Kristo Yesu.  Mwishowe, ndugu, mambo yoyote yenye kuwa ya kweli, mambo yoyote yenye kuwa ya hangaiko nzito, mambo yoyote ya haki, mambo yoyote yenye kuwa safi, mambo yoyote yenye kustahili kupendwa, mambo yoyote yenye kusemwa muzuri, tabia zozote za muzuri, na mambo yoyote yenye kustahili sifa, muendelee kufikiria* mambo hayo.+  Mambo yenye mulijifunza na vilevile mukayakubali na kuyasikia na kuyaona kuhusiana na mimi, muzoee kuyafanya,+ na Mungu wa amani atakuwa pamoja na ninyi. 10  Ninafurahi sana katika Bwana kwamba sasa mwishowe mumeanza tena kunihangaikia.+ Hata kama mulikuwa munanihangaikia, mulikosa nafasi ya kuonyesha jambo hilo. 11  Siseme vile kwa sababu niko katika uhitaji, kwa maana nimejifunza kutosheka hata hali zangu zikuwe namna gani.+ 12  Ninajua namna ya kupungukiwa na chakula+ na namna ya kuwa na vitu vingi. Katika mambo yote na katika hali zote nimejifunza siri ya namna ya kushiba na pia namna ya kuwa na njaa, namna ya kuwa na vitu vingi na pia namna ya kuishi bila kitu. 13  Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia ­nguvu.+ 14  Lakini, mulifanya muzuri kushiriki pamoja na mimi katika taabu yangu. 15  Kwa kweli, ninyi Wafilipi pia munajua kwamba kisha ninyi kujifunza habari njema pale mwanzo, wakati nilitoka Makedonia, hakuna kutaniko lenye lilishiriki pamoja na mimi katika kutoa na kupokea, isipokuwa ninyi tu;+ 16  kwa maana wakati nilikuwa Tesalonike, mulinitumia kitu kwa ajili ya mambo yenye nilikuwa nayo lazima, haikukuwa mara moja tu lakini mara mbili. 17  Haiko kusema ninatafuta zawadi, lakini ninataka matunda yenye kuleta faida zaidi kwenye akiba yenu. 18  Hata hivyo, niko na kila kitu chenye niko nacho lazima, na hata zaidi. Nimejaziwa kila kitu, kwa kuwa sasa nimepokea kutoka kwa Epafrodito+ vitu vyenye mulituma, harufu ya muzuri,+ zabihu yenye kukubaliwa, yenye kumupendeza Mungu. 19  Kwa upande wake Mungu wangu atawajazia kwa ukamili mambo yote yenye muko nayo lazima+ kulingana na utajiri wake katika utukufu kupitia Kristo Yesu. 20  Sasa kwa Mungu na Baba yetu kukuwe utukufu milele na milele. Amina. 21  Mupatie salamu zangu kila mutakatifu katika umoja na Kristo Yesu. Ndugu wenye kuwa pamoja na mimi wanawatumia salamu zao. 22  Watakatifu wote, lakini zaidi wale wa nyumba ya Kaisari,+ wanawatumia ninyi salamu zao. 23  Fazili zenye hazistahiliwe za Bwana Yesu Kristo zikuwe pamoja na roho yenye munaonyesha.

Maelezo ya Chini

Tnn., “mwenzangu kabisa katika nira.”
Ao “wenye wamepambana sana.”
Ao “eko.”
Ao “dua.”
Ao “akili zenu; mawazo yenu.”
Ao “kuwaza juu ya; kutafakari juu ya.”