Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Panga Habari Kulingana na Mapendezi Yako​—Windows

Panga Habari Kulingana na Mapendezi Yako​—Windows

Mambo kadhaa yametiwa katika programu ya JW Library ili ufurahie kusoma. Ili kupata mambo hayo, bonyeza upande wa kulia wa kipanya au telezesha kidole kwenda upande wa chini wa kifaa chako na ufungue Amri za Programu.

Bofya kitufe cha Mengineyo ili upate amri nyingine za programu.

Fuata maelekezo yafuatayo ili kupanga habari kulingana na mapendezi yako:

 Badili Lugha

Unaweza kubadili lugha ya sura au makala unayosoma.

  • Bofya kitufe cha Lugha ili uone ukurasa unaosoma unapatikana katika lugha zipi. Lugha unazotumia mara nyingi zitapangwa juu kwenye orodha hiyo. Toleo lililorahisishwa la Mnara wa Mlinzi pia litapatikana hapa. Unaweza pia kutafuta kwenye orodha hiyo kwa kuandika jina la lugha.

  • Lugha ambazo bado huzijapakuliwa zina alama ya wingu. Bofya lugha ili upakue chapisho. Chapisho litakapopakuliwa kwenye kifaa chako, alama ya wingu itatoweka. Bofya lugha hiyo tena ikiwa unataka kusoma.

 Badili Ukubwa wa Maandishi

Unaweza kubadili ukubwa wa maandishi ili uweze kusoma vizuri.

Bofya kitufe cha Ukubwa wa Herufi; kisha rekebisha kistari kinachotokea ili kuongeza au kupunguza ukubwa wa maandishi. Ukubwa uliochagua utatumika kwa machapisho yote uliyopakua.

 Soma Makala Kama Picha au Kama Maandishi

Unaweza kusoma makala fulani kama picha au kama maandishi. Bofya kitufe kilichoonyeshwa ili kuchagua ungependa kusoma kwa njia gani.

  • Soma Kama Picha: Ukichagua kuisoma kama picha, ukurasa utajitokeza kama ule wa kitabu kilichochapishwa. Wengine hupenda kutumia picha kwa ajili ya machapisho kama vile kitabu cha nyimbo ili waweze kuona alama za muziki.

  • Soma Kama Maandishi: Ukichagua kusoma kama maandishi, maandiko yaliyoonyeshwa yatakuwa na viunganishi unavyoweza kusoma kwa ukubwa uliochagua.

 Fungua Maktaba Kwenye Mtandao

Bonyeza kitufe cha Kufungua Maktaba Kwenye Mtandao ili uweze kufungua habari unayosoma kwenye Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO.

 Tengeneza Takwa Binafsi la Mpangilio wa Biblia

Unapobofya andiko la Biblia katika chapisho, mistari inajitokeza. Bofya kitufe cha Tengeneza Takwa Binafsi kilicho chini ya mistari hiyo ili kuchagua ni tafsiri zipi ungependa zionekane kwenye orodha yako.

Bofya kitufe cha Ongeza au Ondoa ili uongeze au kuondoa tafsiri za Biblia. Bofya Biblia kisha bonyeza kitufe cha kupeleka Juu au Chini ili kupanga orodha.

Ona “Pakua na Utumie Biblia​—Windows” kujifunza jinsi ya kupakua Biblia zaidi katika JW Library.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Machi 2015 kwenye JW Library toleo la 1.4, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa Windows 8.1 au wa karibuni zaidi. Ikiwa huoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—Windows,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.