Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Pakua na Utumie Biblia​—Android

Pakua na Utumie Biblia​—Android

Kusoma na kujifunza Biblia ni sehemu kuu ya JW Library.

Fuata maelekezo yafuatayo ili upakue na kutumia Biblia:

 Pakua Biblia

Unaweza kupakua tafsiri mbalimbali za Biblia ili usome na kujifunza hata unapozima Intaneti.

  • Fungua orodha ya kurambaza, na ubofye Biblia ili kuonyesha orodha ya vitabu vya Biblia.

  • Bofya kitufe cha Lugha ili kuonyesha orodha ya Biblia zilizopo. Tafsiri za lugha unazotumia mara nyingi zitapangwa juu kwenye orodha hiyo. Unaweza pia kutafuta Biblia kwenye orodha hiyo kwa kuandika jina la lugha au Biblia hiyo. Kwa mfano, andika “int” ili upate Biblia ya Kingdom Interlinear ya Kiingereza au “port” ili kupata Biblia zote za Kireno.

  • Biblia ambazo bado hazijapakuliwa zina alama ya wingu. Bofya Biblia ili uipakue. Biblia inapopakuliwa kwenye kifaa chako, alama ya wingu hutoweka. Bofya Biblia hiyo tena ili uisome.

Usipoona tafsiri ya Biblia unayotaka, tafadhali tafuta baadaye. Tafsiri nyingine zitaongezwa kadiri zinavyopatikana.

 Ondoa Biblia

Ikiwa huhitaji tafsiri fulani ya Biblia au ungependa kupata nafasi zaidi kwenye kifaa chako, unaweza kuifuta.

Fungua orodha ya kurambaza na ubofye Biblia, kisha bofya kitufe cha Lugha ili kuonyesha orodha ya Biblia zilizopo. Bofya vitufe vitatu vya Mengineyo vilivyo kwenye Biblia unayotaka kufuta; kisha bofya Ondoa.

 Sasisha Biblia

Mara kwa mara, huenda Biblia uliyopakua ikarekebishwa.

Biblia iliyorekebishwa huwa na alama ya vishale. Unapobofya Biblia hiyo, utaona ujumbe kwamba Biblia hiyo imerekebishwa. Bofya Pakua ili uisasishe, au bofya Baadaye ili uendelee kusoma tafsiri ileile.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Februari 2015 kwenye JW Library toleo la 1.4, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa Android 2.3 au wa karibuni zaidi. Ikiwa huoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—Android,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.