Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 10

Biblia Inaweza Kunisaidiaje?

Biblia Inaweza Kunisaidiaje?

KWA NINI NI MUHIMU

Biblia inasema kwamba “andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Ikiwa hilo ni kweli, basi Biblia inaweza kukupa mwongozo unaohitaji.

WEWE UNGEFANYA NINI?

Fikiria hali hii: David anaendesha gari katika eneo ambalo ni geni kabisa kwake. Ishara za barabarani na maeneo anayoona yanamsadikishia kwamba amepotea. Inaonekana kwamba mahali fulani katika safari yake alifuata barabara isiyofaa.

Ikiwa ungekuwa David, ungefanya nini?

TUA NA UFIKIRI!

Kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua:

  1. Omba mtu akuelekeze.

  2. Angalia ramani, au utumie GPS.

  3. Endelea tu kuendesha gari, ukitumaini kwamba utapata barabara unayoitafuta.

Ni wazi kwamba huenda isifae kuchukua Hatua ya 3.

Hatua ya 2 ina faida kuliko ya kwanza, kwa sababu utakuwa na ramani muda wote wa safari na itakuongoza kadiri unavyosonga.

Biblia inaweza kukusaidia kwa njia hiyo pia!

Kitabu hiki kilichosambazwa sana kinaweza

  • kukuongoza unapokabili matatizo maishani

  • kukusaidia ujielewe vizuri na kuboresha utu wako

  • kukuonyesha jinsi ya kuishi maisha bora zaidi

KUJIBU MASWALI MUHIMU ZAIDI MAISHANI

Tangu tunapoanza kuongea, sisi huuliza maswali.

  • Kwa nini anga ni bluu?

  • Kwa nini nyota zinametameta?

Baadaye tunaanza kujiuliza maswali kuhusu ulimwengu wetu.

Je, inawezekana kwamba majibu ya maswali hayo yamekuwepo sikuzote katika Biblia?

Watu wengi husema kwamba Biblia imejaa hekaya na mafumbo, imepitwa na wakati, au ni ngumu kuielewa. Lakini tatizo liko wapi, je, ni Biblia yenyewe au ni mambo ambayo watu wamesikia kuihusu? Je, wanaweza kuwa wamepotoshwa?

Kwa mfano, watu hufikiri Biblia inasema kwamba Mungu ndiye anayeutawala ulimwengu. Lakini je, huo ndio ukweli wa mambo? Hali katika ulimwengu huu zimeharibika! Ulimwengu umejaa maumivu na watu wanateseka, kuna magonjwa na kifo, umaskini na misiba. Mungu mwenye upendo anawezaje kusababisha mambo hayo yote?

Je, ungependa kupata majibu ya maswali hayo? Huenda ukashangaa kujua Biblia inasema ni nani anayeutawala ulimwengu!

Huenda umetambua kwamba mashauri yanayotolewa katika broshua hii yanategemea Biblia. Mashahidi wa Yehova wanasadiki kwamba Biblia ina mwongozo unaotegemeka. Kwa sababu Biblia yote ‘imeongozwa na roho ya Mungu nayo ni yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.’ (2 Timotheo 3:16, 17) Utafaidika sana kwa kuchunguza kitabu hiki kilichoandikwa zamani lakini kinachofaa hata katika siku zetu!