Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

ilbusca/E+ via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Kwa Nini Watu Hawawezi Kufanya Amani?​—⁠Biblia Inasema Nini?

Kwa Nini Watu Hawawezi Kufanya Amani?​—⁠Biblia Inasema Nini?

 Viongozi wa ulimwengu na mashirika ya kimataifa hayajaweza kuleta amani. Leo kuna mapambano mengi yanayoendelea kuliko wakati mwingine wowote tangu Vita vya Pili vya Ulimwengu vilipokwisha. Watu bilioni mbili hivi, yaani, robo ya idadi ya watu ulimwenguni, wanaishi katika maeneo yaliyoathiriwa na vita.

 Kwa nini wanadamu hawawezi kuleta amani? Biblia inasema nini?

Sababu tatu kwa nini wanadamu hawawezi kutokeza amani

  1.  1. Watu huonyesha mitazamo inayowazuia kujaribu hata kufanya amani. Biblia ilitabiri kwamba katika siku zetu “watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, . . . wasio washikamanifu, . . . wasiotaka makubaliano yoyote, . . . wasiojizuia, wakali, . . . wenye vichwa vigumu, waliojaa kiburi.”​—2 Timotheo 3:2-4.

  2.  2. Wanadamu, wakiwa mmoja mmoja na wakiwa kikundi, hawana uwezo wa kutatua matatizo yao bila msaada wa Muumba wao, Yehova a Mungu. Biblia inafunua kwamba “mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

  3.  3. Ulimwengu huu unadhibitiwa na mtawala mwenye nguvu na mwovu, Shetani Ibilisi, “anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufunuo 12:9) Maadamu “ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu,” kutaendelea kuwa na vita na migogoro.​—1 Yohana 5:19.

Ni nani anayeweza kuleta amani?

 Biblia inatuhakikishia kwamba amani itakuja, si kupitia jitihada za wanadamu, bali italetwa na Mungu.

 Mungu atatimizaje ahadi hiyo? “Mungu anayetoa amani atamponda Shetani.” (Waroma 16:20) Mungu atatumia serikali ya mbinguni, inayotajwa katika Biblia kuwa ni “Ufalme wa Mungu,” ili kutokeza amani ulimwenguni. (Luka 4:43) Chini ya uongozi wa Yesu Kristo, ambaye ndiye Mfalme wa Ufalme huo, watu watajifunza jinsi ya kuishi ya kwa amani.​—Isaya 9:6, 7.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi83:18.