Hamia kwenye habari

Amani Duniani—Kwa Nini Haipatikani?

Amani Duniani—Kwa Nini Haipatikani?

Jibu la Biblia

 Jitihada za wanadamu za kuleta amani hazijawahi kufanikiwa na zitaendelea kutofanikiwa kwa sababu kadhaa:

  •   “Njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake.” (Yeremia 10:23) Wanadamu hawakuumbwa wakiwa na uwezo na pia haki ya kujiongoza, hivyo hawatafanikiwa kupata amani ya kudumu.

  •   “Msiwategemee viongozi wa kibinadamu, hakuna mwanadamu anayeweza kukuokoa. Wanapokufa, wanarudi mavumbini; siku hiyo mipango yao yote inakwisha.” (Zaburi 146:3, 4, Good News Translation) Viongozi wa serikali, hata wale walio na nia nzuri kabisa, hawawezi kutokeza suluhisho la kudumu ili kuondoa chanzo kikuu cha vita.

  •   “Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa . . . wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.” (2 Timotheo 3:1-4) Tunaishi katika “siku za mwisho” za ulimwengu huu mwovu, wakati ambapo mitazamo ya watu inafanya iwe vigumu kupata amani.

  •   “Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ibilisi, ambaye ni adui ya Mungu, ametupwa katika ujirani wa dunia na anawachochea watu wawe na roho kama yake ya ukatili. Mradi anaendelea kuwa “mtawala wa ulimwengu huu,” hatuwezi kamwe kuishi kwa amani.—Yohana 12:31.

  •   “[Ufalme wa Mungu] utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [ambazo zinampinga Mungu], nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu, wala si serikali za kibinadamu, ndio tu utakaotutimizia tamaa yetu ya kupata amani ya kudumu ulimwenguni.—Zaburi 145:16.