Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu Ni Nani?

Mungu Ni Nani?

Watu wengi husema kwamba wanamwamini Mungu. Lakini ukiwauliza Mungu ni nani, utapata majibu tofauti-tofauti. Baadhi yao humwona Mungu kuwa hakimu mkatili ambaye lengo lake ni kuwaadhibu tu watu wanaokosea. Wengine nao hufikiri kwamba, hata wafanye nini, sikuzote Mungu ni mwenye upendo na yuko tayari kuwasamehe. Ilhali wengine wanaamini kwamba Mungu yuko mbali sana na hajali hali yetu ikoje. Kwa kuwa maoni kumhusu Mungu yanatofautiana sana, huenda watu wengi wakahisi kwamba haiwezekani kabisa kumjua.

Je, ni muhimu kumjua Mungu? Ndiyo. Kumjua Mungu vizuri kutafanya maisha yako yawe na kusudi. (Matendo 17:26-28) Kadiri unavyomkaribia, ndivyo atakavyokupenda zaidi na kukusaidia pia. (Yakobo 4:8) Isitoshe, kuwa na ujuzi sahihi kumhusu Mungu kutakuwezesha uishi milele.—Yohana 17:3.

Unaweza kufanya nini ili umjue Mungu? Hebu fikiria kuhusu mtu unayemfahamu vizuri, kama vile rafiki yako wa karibu. Urafiki wenu ulianzaje? Inaelekea ulianza kwa kujua jina lake, sifa zake, mambo anayopenda na asiyopenda, mambo ambayo amefanya na anayopanga kufanya, na kadhalika. Kwa hiyo, ulisitawisha urafiki naye baada ya kujua mambo mbalimbali kumhusu.

Vivyo hivyo, ili tumjue Mungu, tunahitaji kujua mambo yafuatayo kumhusu:

Gazeti hili linafafanua majibu ambayo Biblia inatoa kuhusu maswali hayo. Litakusaidia kumjua Mungu na pia utajifunza faida za kusitawisha uhusiano wa karibu na yeye.