Barua ya Yakobo 4:1-17

  • Usiwe rafiki ya ulimwengu (1-12)

    • Mpingeni Ibilisi (7)

    • Mkaribieni Mungu (8)

  • Onyo dhidi ya kiburi (13-17)

    • “Yehova akipenda” (15)

4  Ni nini chanzo cha vita na mapigano miongoni mwenu? Je, havitokani na tamaa zenu za mwili zinazoendeleza pambano ndani yenu?*+  Mnatamani, lakini hamna kitu. Mnaendelea kuua na kutamani kwa wivu, na bado hamwezi kupata. Mnaendelea kupigana na kufanya vita.+ Hamna kitu kwa sababu hamwombi.  Mnapoomba, hampokei kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya, ili mvitumie kwa ajili ya tamaa zenu za mwili.  Enyi wazinzi,* je, hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu? Kwa hiyo, yeyote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.+  Au je, mnafikiri kwamba andiko linasema hivi bila sababu: “Roho ambayo imekaa ndani yetu huendelea kutamani kwa wivu”?+  Hata hivyo, fadhili zisizostahiliwa ambazo Yeye hutoa ni kubwa zaidi. Kwa hiyo, linasema: “Mungu huwapinga wenye majivuno,+ lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”+  Basi, jitiisheni kwa Mungu;+ lakini mpingeni Ibilisi,+ naye atawakimbia ninyi.+  Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.+ Safisheni mikono yenu, ninyi watenda dhambi,+ na takaseni mioyo yenu,+ ninyi mnaositasita.  Iweni na taabu na mwomboleze na kulia.+ Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa maombolezo, na badala ya kuwa na shangwe mkate tamaa. 10  Jinyenyekezeni machoni pa Yehova,*+ naye atawainua.+ 11  Akina ndugu acheni kusemana kati yenu.+ Yeyote anayemsema vibaya ndugu au anayemhukumu ndugu yake husema vibaya juu ya sheria na kuihukumu sheria. Na ikiwa unaihukumu sheria, basi wewe si mtendaji wa sheria, bali ni mwamuzi. 12  Kuna mmoja tu ambaye ni Mpaji-sheria na Mwamuzi,+ yule anayeweza kuokoa na kuangamiza.+ Lakini wewe ni nani ili umhukumu jirani yako?+ 13  Haya, basi, ninyi mnaosema: “Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,”+ 14  ingawa hamjui jinsi maisha yenu yatakavyokuwa kesho.+ Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka.+ 15  Badala yake, mnapaswa kusema: “Yehova* akipenda,+ tutaishi na kufanya hili au lile.” 16  Lakini sasa mnajivuna na kujigamba kwa kiburi. Majivuno yote ya namna hiyo ni maovu. 17  Kwa hiyo, ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ndani ya viungo vyenu.”
Au “ Enyi msio waaminifu.”