Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

AMKENI! Na. 1 2018 | Njia ya Maisha Inayoleta Furaha

TUNAWEZA KUPATA WAPI MWONGOZO WENYE KUTEGEMEKA WA KUISHI MAISHA YENYE FURAHA?

Biblia inasema hivi: “Wenye furaha ni wale wasio na lawama katika njia yao.”​—Zaburi 119:1.

Makala hizi saba zinazungumzia kanuni ambazo zimetumiwa kwa muda mrefu na kuthibitika kuwa na uwezo wa kuleta furaha maishani.

 

Kuipata Njia Hiyo

Je, unajiona kuwa mtu mwenye furaha? Ni mambo gani yanayoleta furaha?

Kuridhika na Kuwa Mkarimu

Watu wengi hufikiri kwamba furaha hutokana na mali na utajiri. Je, kweli pesa na vitu vya kimwili huleta furaha ya kudumu? Uthibitisho unafunua nini?

Afya Nzuri na Ustahimilivu

Je, kuzorota kwa afya kunafanya mtu asiweze kabisa kuwa na furaha?

Upendo

Kuwapenda wengine, na kuonyeshwa upendo huchangia kwa kiwango kikubwa kuleta furaha.

Kusamehe

Maisha yaliyojaa hasira na chuki humzuia mtu kuwa na furaha na huathiri afya pia.

Kuwa na Kusudi la Maisha

Kupata majibu yenye kuridhisha kuhusu maswali muhimu maishani huchangia kuleta furaha.

Tumaini

Si rahisi kwa wengi kuwa na furaha ikiwa hawajui maisha yao na ya wale wanaowapenda yatakuwaje wakati ujao.

Jifunze Mengi Zaidi

Kuna mambo mengi yanayoweza kumfanya mtu awe na furaha au asiwe na furaha. Soma upate habari kuhusu tovuti isiyotoza gharama yoyote inayoweza kukusaidia ujue jinsi ya kushughulikia mambo muhimu maishani mwako.