Zaburi 55:1-23

  • Sala ya mtu aliyesalitiwa na rafiki

    • Adhihakiwa na rafiki wa karibu (12-14)

    • “Mtupie Yehova mzigo wako” (22)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi. 55  Sikiliza sala yangu, Ee Mungu,+Na usiipuuze sala yangu ya kuomba rehema.*+   Nisikilize na unijibu.+ Hangaiko langu linanisumbua,+Nami nimefadhaika   Kwa sababu ya mambo ambayo adui anasemaNa mkazo kutoka kwa mwovu. Kwa maana wananirundikia taabu,Na kwa hasira wana chuki kali kunielekea.+   Moyo wangu una maumivu makali,+Na hofu ya kifo inanilemea.+   Hofu na kutetemeka hunijia,Na woga hunishika.   Daima ninasema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa! Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.   Tazama! Ningekimbia na kwenda mbali sana.+ Ningekaa nyikani.+ (Sela)   Ningeenda haraka mahali pa kujifichaMbali na upepo mkali, mbali na dhoruba.”   Wavuruge, Ee Yehova, na uvuruge mipango yao,*+Kwa maana nimeona ukatili na mizozo jijini. 10  Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake;Ndani yake kuna fitina na taabu.+ 11  Uharibifu uko ndani yake;Ukandamizaji na udanganyifu hauondoki kamwe katika uwanja wake.+ 12  Kwa maana si adui anayenidhihaki;+La sivyo ningevumilia. Si adui aliyeinuka dhidi yangu;La sivyo ningeweza kujificha. 13  Lakini ni wewe, mwanadamu kama mimi,*+Rafiki yangu mwenyewe ninayemjua vizuri.+ 14  Tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki wa karibu sana;Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tukitembea pamoja na umati. 15  Na wapatwe na maangamizi!+ Na washuke Kaburini* wakiwa hai;Kwa maana uovu hukaa miongoni mwao na ndani yao. 16  Lakini mimi, nitamlilia Mungu,Na Yehova ataniokoa.+ 17  Jioni na asubuhi na adhuhuri, ninahangaika na kulia kwa uchungu,*+Naye huisikia sauti yangu.+ 18  Ataniokoa* na kunipa amani mbali na wale wanaopigana nami,Kwa maana umati huja kunishambulia.+ 19  Mungu atasikia na kukabiliana nao,+Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme tangu zamani.+ (Sela) Watakataa kubadilika,Wale ambao hawajamwogopa Mungu.+ 20  Aliwashambulia* walio na amani pamoja naye;+Alilivunja agano lake.+ 21  Maneno yake ni laini kuliko siagi,+Lakini mzozo umo moyoni mwake. Maneno yake ni laini kuliko mafuta,Lakini ni panga zilizochomolewa.+ 22  Mtupie Yehova mzigo wako,+Naye atakutegemeza.+ Hataruhusu kamwe mwadilifu aanguke.*+ 23  Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo lenye kina kabisa.+ Watu hao wenye hatia ya damu ambao ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+ Lakini mimi, nitakutumaini wewe.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “Na usijifiche ninaposali kukuomba msaada.”
Tnn., “ugawanye ndimi zao.”
Au “mwanadamu, mtu tunayelingana.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “nimevurugika.”
Tnn., “Atanikomboa.”
Yaani, rafiki yake wa zamani anayetajwa katika mstari wa 13 na 14.
Au “ayumbeyumbe; apepesuke.”