Zaburi 130:1-8

  • “Kutoka vilindini ninakulilia”

    • ‘Ikiwa ungekuwa unatazama makosa’ (3)

    • Msamaha wa kweli hutoka kwa Yehova (4)

    • “Ninamngojea Yehova kwa hamu” (6)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 130  Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Yehova.+   Ee Yehova, isikie sauti yangu. Masikio yako na yasikilize sihi zangu za kuomba msaada.   Ikiwa ungekuwa unatazama* tu makosa, Ee Yah,*Basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?+   Kwa maana wewe hutoa msamaha wa kweli,+Ili watu wakuhofu.*+   Ninamtumaini Yehova, nafsi yangu yote inamtumaini;Ninangoja neno lake.   Ninamngojea Yehova kwa hamu,+Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+Naam, kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi.   Watu wa Israeli na waendelee kumngojea Yehova,Kwa maana Yehova ni mshikamanifu katika upendo wake,+Naye ana nguvu nyingi za kukomboa.   Atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika makosa yao yote.

Maelezo ya Chini

Au “unafuatilia.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “Ili uogopwe.”