Methali 13:1-25
13 Mwana mwenye hekima hukubali nidhamu ya baba yake,+Lakini mwenye dhihaka hasikilizi kemeo.*+
2 Mtu atakula mema kwa sababu ya matunda ya maneno yake,*+Lakini tamaa hasa* ya wenye hila ni ukatili.
3 Anayelinda kinywa chake anaulinda uhai wake,*+Lakini anayefungua wazi midomo yake ataangamia.+
4 Kuna vitu anavyotamani sana mtu mvivu, ingawa hana chochote,+Lakini mwenye bidii atatoshelezwa kikamili.*+
5 Mwadilifu huchukia uwongo,+Lakini matendo ya waovu huleta aibu na fedheha.
6 Uadilifu humlinda mtu ambaye njia yake haina hatia,+Lakini uovu humshusha mtenda dhambi.
7 Kuna mtu anayejifanya tajiri ingawa hana chochote;+Kuna mtu anayejifanya maskini ingawa ana mali nyingi.
8 Utajiri ni fidia ya uhai wa mtu,+Lakini maskini hata hawatishwi.*+
9 Nuru ya waadilifu hung’aa kwa uangavu,*+Lakini taa ya waovu itazimwa.+
10 Kimbelembele husababisha mzozo tu,+Lakini hekima ni ya wale wanaotafuta ushauri.*+
11 Mali inayopatikana haraka* itapungua,+Lakini mali ya yule anayeikusanya kidogo kidogo* itaongezeka.
12 Matarajio yaliyoahirishwa* hufanya moyo uwe mgonjwa,+Lakini tamaa inayotoshelezwa ni mti wa uzima.+
13 Yeyote anayedharau mafundisho* atalipia adhabu yake,+Lakini anayeheshimu amri atathawabishwa.+
14 Mafundisho* ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima+Humwepusha mtu na mitego ya kifo.
15 Ufahamu ulio makini huleta kibali,Lakini njia ya wenye hila ni ngumu sana.
16 Mtu mwerevu hutenda kwa ujuzi,+Lakini mjinga hufunua ujinga wake mwenyewe.+
17 Mjumbe mwovu huanguka taabani,+Lakini mjumbe mwaminifu huleta maponyo.+
18 Yeyote anayepuuza nidhamu huwa maskini na kupata aibu,Lakini anayekubali kurekebishwa* atatukuzwa.+
19 Tamaa inapotoshelezwa ni tamu kwa mtu,*+Lakini wapumbavu huchukia kuacha uovu.+
20 Anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima,+Lakini anayeshirikiana na wapumbavu ataumia.+
21 Msiba huwafuatia watenda dhambi,+Lakini ufanisi huwathawabisha waadilifu.+
22 Mtu mwema huwaachia urithi wajukuu wake,Lakini mali ya mtenda dhambi itawekwa akiba kwa ajili ya mwadilifu.+
23 Shamba la maskini lililolimwa huzaa chakula kingi,Lakini linaweza* kufagiliwa mbali na ukosefu wa haki.
24 Yeyote anayeizuia fimbo yake* anamchukia mwanawe,+Lakini yule anayempenda humtia nidhamu kwa bidii.*+
25 Mwadilifu hula na kutosheleza hamu* yake,+Lakini tumbo la waovu liko tupu.+
Maelezo ya Chini
^ Au “rekebisho.”
^ Tnn., “kinywa chake.”
^ Au “Lakini nafsi hasa.”
^ Au “anailinda nafsi yake.”
^ Tnn., “atanenepeshwa.”
^ Tnn., “hawasikii kemeo lolote.”
^ Tnn., “hushangilia.”
^ Au “wanaoshauriana.”
^ Au “Mali inayotokana na ubatili.”
^ Tnn., “anayekusanya kwa mkono.”
^ Au “Tumaini lililoahirishwa.”
^ Au “neno.”
^ Au “Sheria.”
^ Au “karipio.”
^ Au “nafsi.”
^ Au “anaweza.”
^ Au “asiyetoa nidhamu; adhabu.”
^ Au labda, “bila kukawia.”
^ Au “nafsi.”