Methali 13:1-25

  • Wanaotafuta ushauri wana hekima (10)

  • Tumaini likikawia huufanya moyo uwe mgonjwa (12)

  • Mjumbe mwaminifu huleta maponyo (17)

  • Kutembea na wenye hekima humfanya mtu awe na hekima (20)

  • Nidhamu huonyesha upendo (24)

13  Mwana mwenye hekima hukubali nidhamu ya baba yake,+Lakini mwenye dhihaka hasikilizi kemeo.*+   Mtu atakula mema kwa sababu ya matunda ya maneno yake,*+Lakini tamaa hasa* ya wenye hila ni ukatili.   Anayelinda kinywa chake anaulinda uhai wake,*+Lakini anayefungua wazi midomo yake ataangamia.+   Kuna vitu anavyotamani sana mtu mvivu, ingawa hana chochote,+Lakini mwenye bidii atatoshelezwa kikamili.*+   Mwadilifu huchukia uwongo,+Lakini matendo ya waovu huleta aibu na fedheha.   Uadilifu humlinda mtu ambaye njia yake haina hatia,+Lakini uovu humshusha mtenda dhambi.   Kuna mtu anayejifanya tajiri ingawa hana chochote;+Kuna mtu anayejifanya maskini ingawa ana mali nyingi.   Utajiri ni fidia ya uhai wa mtu,+Lakini maskini hata hawatishwi.*+   Nuru ya waadilifu hung’aa kwa uangavu,*+Lakini taa ya waovu itazimwa.+ 10  Kimbelembele husababisha mzozo tu,+Lakini hekima ni ya wale wanaotafuta ushauri.*+ 11  Mali inayopatikana haraka* itapungua,+Lakini mali ya yule anayeikusanya kidogo kidogo* itaongezeka. 12  Matarajio yaliyoahirishwa* hufanya moyo uwe mgonjwa,+Lakini tamaa inayotoshelezwa ni mti wa uzima.+ 13  Yeyote anayedharau mafundisho* atalipia adhabu yake,+Lakini anayeheshimu amri atathawabishwa.+ 14  Mafundisho* ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima+Humwepusha mtu na mitego ya kifo. 15  Ufahamu ulio makini huleta kibali,Lakini njia ya wenye hila ni ngumu sana. 16  Mtu mwerevu hutenda kwa ujuzi,+Lakini mjinga hufunua ujinga wake mwenyewe.+ 17  Mjumbe mwovu huanguka taabani,+Lakini mjumbe mwaminifu huleta maponyo.+ 18  Yeyote anayepuuza nidhamu huwa maskini na kupata aibu,Lakini anayekubali kurekebishwa* atatukuzwa.+ 19  Tamaa inapotoshelezwa ni tamu kwa mtu,*+Lakini wapumbavu huchukia kuacha uovu.+ 20  Anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima,+Lakini anayeshirikiana na wapumbavu ataumia.+ 21  Msiba huwafuatia watenda dhambi,+Lakini ufanisi huwathawabisha waadilifu.+ 22  Mtu mwema huwaachia urithi wajukuu wake,Lakini mali ya mtenda dhambi itawekwa akiba kwa ajili ya mwadilifu.+ 23  Shamba la maskini lililolimwa huzaa chakula kingi,Lakini linaweza* kufagiliwa mbali na ukosefu wa haki. 24  Yeyote anayeizuia fimbo yake* anamchukia mwanawe,+Lakini yule anayempenda humtia nidhamu kwa bidii.*+ 25  Mwadilifu hula na kutosheleza hamu* yake,+Lakini tumbo la waovu liko tupu.+

Maelezo ya Chini

Au “rekebisho.”
Tnn., “kinywa chake.”
Au “Lakini nafsi hasa.”
Au “anailinda nafsi yake.”
Tnn., “atanenepeshwa.”
Tnn., “hawasikii kemeo lolote.”
Tnn., “hushangilia.”
Au “wanaoshauriana.”
Au “Mali inayotokana na ubatili.”
Tnn., “anayekusanya kwa mkono.”
Au “Tumaini lililoahirishwa.”
Au “neno.”
Au “Sheria.”
Au “karipio.”
Au “nafsi.”
Au “anaweza.”
Au “asiyetoa nidhamu; adhabu.”
Au labda, “bila kukawia.”
Au “nafsi.”