Methali 12:1-28

  • Anayechukia karipio hana akili (1)

  • “Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga” (18)

  • Kusitawisha amani huleta shangwe (20)

  • Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova (22)

  • Mahangaiko huulemea moyo (25)

12  Anayependa nidhamu anapenda ujuzi,+Lakini anayechukia karipio hana akili.*+   Mtu mwema hupata kibali cha Yehova,Lakini Yeye humhukumu mtu anayepanga njama za uovu.+   Hakuna mtu anayekuwa salama kwa kutenda uovu,+Lakini waadilifu hawatang’olewa kamwe.   Mke mwema* ni taji kwa mume wake,+Lakini mke anayetenda kwa aibu ni kama uozo katika mifupa ya mume wake.+   Mawazo ya waadilifu ni ya haki,Lakini mwongozo wa waovu hudanganya.   Maneno ya waovu huvizia ili kuua,*+Lakini kinywa cha wanyoofu huwaokoa.+   Waovu wanapoangamizwa, hawako tena,Lakini nyumba ya mwadilifu itaendelea kusimama.+   Mtu husifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+Lakini mtu aliye na moyo uliopotoka atatendewa kwa dharau.+   Ni afadhali usiheshimiwe sana lakini uwe na mtumishiKuliko kujitukuza mwenyewe na ukose chakula.*+ 10  Mwadilifu huwatunza wanyama anaowafuga,*+Lakini hata rehema ya waovu ni ukatili. 11  Anayelima shamba lake atakuwa na chakula tele,+Lakini anayefuatia vitu visivyo na maana hana busara.* 12  Mtu mwovu hutamani kitu kilichokamatwa na watu wengine waovu,Lakini mzizi wa waadilifu huzaa matunda. 13  Mwovu hunaswa na mazungumzo yake ya dhambi,+Lakini mwadilifu huokoka kutoka katika taabu. 14  Mtu hushiba mema kwa sababu ya matunda ya maneno yake,*+Na kazi ya mikono yake itamthawabisha. 15  Njia ya mpumbavu ni sawa machoni pake mwenyewe,+Lakini mwenye hekima hukubali ushauri.*+ 16  Mjinga huonyesha papo hapo* kwamba ameudhika,+Lakini mtu mwerevu hupuuza* matusi. 17  Anayetoa ushahidi kwa uaminifu atasema ukweli,*Lakini shahidi wa uwongo husema mambo ya udanganyifu. 18  Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga,Lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.+ 19  Midomo inayosema ukweli itadumu milele,+Lakini ulimi unaosema uwongo utadumu kwa muda mfupi tu.+ 20  Udanganyifu umo moyoni mwa wale wanaopanga njama zinazodhuru,Lakini wale wanaositawisha* amani wana shangwe.+ 21  Hakuna madhara yatakayompata mwadilifu,+Lakini waovu watapatwa na misiba mingi.+ 22  Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova,+Lakini wanaotenda kwa uaminifu humfurahisha. 23  Mtu mwerevu hufunika mambo anayojua,Lakini moyo wa mjinga hububujika ujinga.+ 24  Mkono wa wenye bidii utatawala,+Lakini mikono milegevu italazimishwa kufanya kazi za utumwa.+ 25  Mahangaiko yaliyo moyoni mwa mtu huulemea moyo,*+Lakini neno jema huuchangamsha.+ 26  Mwadilifu hutafuta malisho yake,Lakini njia ya waovu huwapotosha. 27  Watu wavivu hawakimbizi mawindo,+Lakini bidii ni hazina ya mtu yenye thamani. 28  Kijia cha uadilifu huongoza kwenye uzima;+Kando ya kijia hicho hakuna kifo.

Maelezo ya Chini

Au “hana ufahamu.”
Au “mwenye uwezo.”
Tnn., “huvizia ili kumwaga damu.”
Tnn., “mkate.”
Au “huitunza nafsi ya mnyama anayemfuga.”
Tnn., “amepungukiwa moyoni.”
Tnn., “kinywa chake.”
Au “mashauri.”
Au “siku hiyohiyo.”
Tnn., “hufunika.”
Tnn., “mambo ya uadilifu.”
Tnn., “Lakini washauri wa.”
Au “humfanya ashuke moyo.”