Kulingana na Luka 1:1-80

  • Ujumbe kwa Theofilo (1-4)

  • Gabrieli atabiri kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji (5-25)

  • Gabrieli atabiri kuzaliwa kwa Yesu  (26-38)

  • Maria amtembelea Elisabeti (39-45)

  • Maria amtukuza Yehova (46-56)

  • Yohana azaliwa na kupewa jina (57-66)

  • Unabii wa Zekaria (67-80)

1  Kwa kuwa watu wengi wamejitahidi kukusanya habari kuhusu mambo ambayo tunayasadiki kabisa,+  kama tulivyoyapokea kutoka kwa wale waliokuwa mashahidi wa kujionea tangu mwanzo+ na wahudumu wa ujumbe,+  mheshimiwa Theofilo,+ mimi pia nimefuatilia mambo yote kwa usahihi tangu mwanzo, nami nimeamua kukuandikia mambo hayo kwa utaratibu mzuri,  ili ujue kikamili uhakika wa mambo uliyofundishwa kwa mdomo.+  Katika siku za Herode,*+ mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani aliyeitwa Zekaria wa kikundi cha Abiya.+ Mke wake aliitwa Elisabeti na alikuwa wa ukoo wa Haruni.  Wote wawili walikuwa waadilifu mbele za Mungu na walitembea bila lawama kulingana na amri na sheria zote za Yehova.*  Lakini hawakuwa na mtoto, kwa sababu Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili walikuwa wamezeeka.  Alipokuwa akihudumu akiwa kuhani mbele za Mungu wakati wa zamu ya kikundi chake,+  kulingana na desturi ya* ukuhani zamu yake ikafika ya kuingia patakatifu pa Yehova*+ ili kufukiza uvumba.+ 10  Umati wote ulikuwa nje ukisali saa hiyo ya kufukiza uvumba. 11  Malaika wa Yehova* akamtokea, akiwa amesimama upande wa kulia wa madhabahu ya uvumba. 12  Lakini Zekaria alihangaishwa na jambo aliloona, akaogopa sana. 13  Hata hivyo, malaika akamwambia: “Usiogope, Zekaria, kwa sababu dua yako imesikiwa vema, na mke wako Elisabeti atakuzalia mwana, nawe utamwita Yohana.+ 14  Utakuwa na shangwe na furaha nyingi, na wengi watashangilia atakapozaliwa,+ 15  kwa maana atakuwa mkuu mbele za Yehova.*+ Lakini hapaswi kamwe kunywa divai wala kileo,+ naye atajazwa roho takatifu hata kabla ya kuzaliwa,*+ 16  naye atawarudisha wana wengi wa Israeli kwa Yehova* Mungu wao.+ 17  Pia, atamtangulia kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo ya akina baba kwa watoto+ na wale wasiotii kwenye hekima ya waadilifu, na kumwandalia Yehova* watu waliotayarishwa.”+ 18  Zekaria akamuuliza malaika: “Ninawezaje kuwa na uhakika kuhusu jambo hili? Kwa maana nimezeeka, nao umri wa mke wangu pia umesonga.” 19  Malaika akamjibu: “Mimi ni Gabrieli,+ ninayesimama karibu mbele za Mungu,+ nami nilitumwa nizungumze nawe na kukutangazia habari hii njema. 20  Lakini tazama! utakaa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ambayo mambo hayo yatatendeka, kwa sababu hukuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa katika wakati uliowekwa.” 21  Watu wakaendelea kumsubiri Zekaria, nao wakashangaa kwa sababu alikuwa amekawia sana katika patakatifu. 22  Alipotoka hakuweza kuzungumza nao, basi wakajua kwamba alikuwa ameona jambo la kustaajabisha* katika patakatifu. Akaendelea kuwafanyia ishara lakini hakuweza kuongea. 23  Siku zake za utumishi mtakatifu* zilipokwisha, akarudi nyumbani. 24  Baada ya siku chache Elisabeti mke wake akapata mimba, naye hakutoka nyumbani kwa miezi mitano. Alikuwa akisema: 25  “Yehova* amenitendea hivi katika siku hizi. Amenikumbuka ili kuniondolea aibu kati ya watu.”+ 26  Katika mwezi wake wa sita, malaika Gabrieli+ akatumwa na Mungu aende katika jiji la Nazareti huko Galilaya, 27  kwa bikira+ aliyeitwa Maria,+ mchumba wa mwanamume aliyeitwa Yosefu wa nyumba ya Daudi. 28  Malaika akaja na kumwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa sana, Yehova* yuko pamoja nawe.” 29  Lakini Maria akahangaishwa sana na maneno aliyoambiwa, naye akaanza kufikiria maana ya salamu hizo. 30  Basi malaika akamwambia: “Usiogope, Maria, kwa maana umepata kibali cha Mungu. 31  Tazama! utapata mimba* na kuzaa mwana+ nawe utamwita Yesu.+ 32  Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33  naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+ 34  Lakini Maria akamuuliza malaika: “Hilo litawezekanaje, kwa kuwa sina uhusiano wa kingono na mwanamume?”+ 35  Malaika akamjibu: “Roho takatifu itakuja juu yako,+ na nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa hiyo yule atakayezaliwa ataitwa mtakatifu,+ Mwana wa Mungu.+ 36  Tazama! Hata Elisabeti mtu wako wa ukoo, ingawa amezeeka ana mimba ya miezi sita, yule anayejulikana kuwa tasa; 37  kwa sababu kwa Mungu hakuna tangazo* lisilowezekana.”+ 38  Ndipo Maria akasema: “Tazama! Kijakazi wa Yehova!* Na itendeke kwangu kulingana na tangazo lako.” Kisha malaika akaondoka. 39  Basi siku hizo, Maria akafunga safari haraka kwenda kwenye eneo lenye milima, mpaka jiji fulani la Yuda, 40  naye akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elisabeti. 41  Elisabeti aliposikia salamu za Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka, naye Elisabeti akajazwa roho takatifu 42  na kusema kwa sauti kubwa: “Umebarikiwa kati ya wanawake, na uzao wa tumbo lako umebarikiwa! 43  Imekuwaje nimependelewa hivi kwamba mama ya Bwana wangu amenitembelea? 44  Kwa maana tazama! niliposikia salamu zako, mtoto aliye tumboni mwangu aliruka kwa shangwe. 45  Mwenye furaha pia ni yule aliyeamini, kwa sababu atatimiziwa kikamili mambo aliyoambiwa kutoka kwa Yehova.”* 46  Naye Maria akasema: “Nafsi* yangu inamtukuza Yehova,*+ 47  na roho yangu haitaacha kumshangilia Mungu Mwokozi wangu,+ 48  kwa sababu ametazama hali ya chini ya kijakazi wake.+ Tazama! tangu sasa vizazi vyote vitanitangaza kuwa mwenye furaha,+ 49  kwa sababu Mwenye nguvu amenitendea mambo makuu, nalo jina lake ni takatifu,+ 50  naye huwaonyesha rehema wale wanaomwogopa, kizazi baada ya kizazi.+ 51  Amefanya mambo makuu kwa mkono wake, amewatawanya wenye majivuno katika nia ya mioyo yao.+ 52  Amewashusha watu wenye nguvu kutoka kwenye viti vya ufalme+ na kuwainua watu wa hali ya chini;+ 53  amewashibisha kabisa wenye njaa kwa vitu vyema+ na kuwafukuza mikono mitupu wale waliokuwa na mali. 54  Amekuja kumsaidia Israeli mtumishi wake, amekumbuka rehema zake,+ 55  kama alivyowaahidi mababu zetu, Abrahamu na uzao wake,*+ milele.” 56  Maria akakaa na Elisabeti kwa karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake. 57  Wakati wa Elisabeti wa kujifungua ukafika, naye akazaa mtoto wa kiume. 58  Majirani na watu wake wa ukoo wakasikia kwamba Yehova* amemwonyesha rehema nyingi, wakafurahi pamoja naye.+ 59  Siku ya nane wakaja kumtahiri huyo mtoto,+ nao walitaka kumpa jina la baba yake, Zekaria. 60  Lakini mama yake akajibu: “Hapana! ataitwa Yohana.” 61  Wakamwambia: “Hakuna mtu wenu wa ukoo anayeitwa jina hilo.” 62  Kisha wakamuuliza baba yake wakitumia ishara jina alilotaka kumpa. 63  Basi akaomba kibao akaandika: “Yohana ndilo jina lake.”+ Ndipo wote wakashangaa. 64  Mara moja kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukawekwa huru, akaanza kuongea,+ akimsifu Mungu. 65  Majirani wao wote wakaogopa, na mambo yote hayo yakaanza kuzungumziwa katika eneo lote la milimani la Yudea. 66  Wote waliosikia mambo hayo wakayaweka moyoni, wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa aina gani?” Kwa maana mkono wa Yehova* ulikuwa pamoja naye. 67  Kisha Zekaria baba yake akajazwa roho takatifu, naye akatoa unabii huu: 68  “Asifiwe Yehova* Mungu wa Israeli,+ kwa sababu amewakumbuka watu wake na kuwaletea ukombozi.+ 69  Naye ametuinulia pembe ya wokovu*+ katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,+ 70  kama alivyosema kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu tangu zamani,+ 71  kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia;+ 72  ili kuonyesha rehema kuhusiana na mababu zetu na kulikumbuka agano lake takatifu,+ 73  kama alivyomwapia Abrahamu babu yetu,+ 74  kwamba atatukomboa kutoka mikononi mwa adui, na kutupatia pendeleo la kumtolea utumishi mtakatifu bila woga 75  kwa ushikamanifu na uadilifu mbele zake siku zetu zote. 76  Lakini wewe, mtoto mchanga, utaitwa nabii wa Aliye Juu Zaidi, kwa maana utaenda mbele za Yehova* ili kutayarisha njia zake,+ 77  kuwapa watu wake ujuzi wa wokovu kupitia kusamehewa dhambi zao,+ 78  kwa sababu ya huruma nyororo za Mungu wetu. Kwa huruma hizo tutapata mapambazuko kutoka juu, 79  ili kuwapa nuru wale wanaokaa gizani na katika kivuli cha kifo+ na kuongoza hatua zetu kwenye njia ya amani.” 80  Yule mtoto akakua na kupata nguvu katika roho, naye aliishi jangwani mpaka siku aliyojionyesha waziwazi kwa Israeli.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “zoea la.”
Au “tangu akiwa katika tumbo la mama yake.”
Au “maono.”
Au “utumishi wake wa watu wote.”
Au “utachukua mimba katika tumbo lako la uzazi.”
Au “jambo lolote.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “mbegu yake.”
Au “mwokozi mwenye nguvu.” Angalia Kamusi, “Pembe.”