Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Mungu anasikiliza sala zote?

Mungu anasikiliza watu wa mataifa yote. (Zaburi 145:18, 19) Neno lake, Biblia, linatutia moyo tuzungumuze naye juu ya jambo lolote linalotuhangaisha. (Wafilipi 4:6, 7) Hata hivyo, sala fulani hazimupendeze Mungu. Kwa mufano, sala za kurudilia-rudilia zilizowekwa katika akili hazimupendeze.​—Soma Mathayo 6:7.

Pia, Yehova anachukia sala za watu ambao wanavunja sheria zake kimakusudi. (Methali 28:9) Kwa mufano, nyakati za zamani, Mungu alikataa kuwasikiliza Waisraeli waliokuwa na hatia ya uuaji. Ni wazi kwamba tunapaswa kutimiza mambo fulani ili Mungu asikilize sala zetu.​—Soma Isaya 1:15.

Tunapaswa kufanya nini ili Mungu asikilize sala zetu?

Hatuwezi kumukaribia Mungu katika sala bila imani. (Yakobo 1:5, 6) Tunapaswa kuwa na uhakika kwamba Mungu yuko na kwamba anatuhangaikia. Tunaweza kufanya imani yetu iwe yenye nguvu kwa kujifunza Biblia kwa sababu imani ya kweli inategemea mambo ya kweli na usadikisho unaopatikana katika Neno la Mungu.​—Soma Waebrania 11:1, 6.

Tunapaswa kusali kwa moyo wote na kwa unyenyekevu. Hata Yesu, Mwana wa Mungu, alikuwa munyenyekevu aliposali. (Luka 22:41, 42) Kwa hiyo, kuliko kumuambia Mungu jambo la kufanya, tunapaswa kujikaza kuelewa mambo ambayo anatuomba tufanye kwa kusoma Biblia. Kwa kufanya hivyo tunaweza kusali kupatana na mapenzi ya Mungu.​—Soma 1 Yohana 5:14.