Ona video zinazopatikana

Je, Mashahidi wa Yehova Wanakataa Wale Waliokuwa Katika Dini Yao Zamani?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanakataa Wale Waliokuwa Katika Dini Yao Zamani?

 Sisi hatukatae wale Mashahidi wa Yehova wenye kubatizwa lakini ambao hawahubiri tena, labda hata wamejitenga na waamini wenzao. Lakini, tunawatafuta na kujaribu kuwasaidia wapendezwe tena na mambo ya Mungu.

 Sikusema kwamba mutu anapofanya zambi nzito anatengwa mara moja. Hata hivyo, ikiwa Shahidi aliyebatizwa anazoea kuvunja kanuni za Biblia na hapende kutubu, yeye anatengwa. Biblia inasema waziwazi hivi: ‘Ondoeni yule mutu muovu kati yenu.’—1 Wakorintho 5:13.

 Namna gani ikiwa bwana anatengwa na kutaniko, lakini bibi yake na watoto wake wangali Mashahidi wa Yehova? Yeye anabaki tu bwana na baba katika familia yake, lakini haweze tena kushirikiana nao katika mambo ya kiroho. Uhusiano wa ndoa kati yake na bibi yake utaendelea na ataendelea kuhangaikia mahitaji ya kimwili ya familia yake.

 Watu ambao wametengwa na kutaniko wanaweza kuhuzuria mikutano yetu. Ikiwa wanataka, wanaweza pia kupokea mashauri ya wazee wa kutaniko. Kusudi la wazee ni kusaidia kila mutu aliyetengwa astahili tena kuwa Shahidi wa Yehova. Mutu aliyetengwa anayeacha mwenendo mubaya na anayeonyesha kabisa kwamba anataka kuishi kulingana na kanuni za Biblia anakaribishwa tena katika kutaniko.