Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wana Makasisi Wanaolipwa?

Je, Mashahidi wa Yehova Wana Makasisi Wanaolipwa?

 Wakiiga mfano wa Wakristo katika karne ya kwanza, Mashahidi wa Yehova hawana tofauti kati ya makasisi na waumini. Mashahidi wote waliobatizwa ni wahudumu waliowekwa rasmi kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Mashahidi wamepangwa katika makutaniko ya watu 100 hivi. Wanaume waliokomaa kiroho katika kila kutaniko hutumika kama “wanaume wazee,” au wazee wa kutaniko. (Tito 1:5) Wao hufanya hivyo bila kulipwa.