Hamia kwenye habari

BIBLIA INABADILI MAISHA

Walipata ‘Lulu Yenye Thamani Kubwa’

Walipata ‘Lulu Yenye Thamani Kubwa’

 Yesu alifundisha kwamba Ufalme wa Mungu utasuluhisha matatizo yote ya wanadamu. (Mathayo 6:10) Kwenye Mathayo 13:44-46, alitoa mifano miwili ili kuonyesha thamani ya kweli kuhusu Ufalme wa Mungu:

  •   Mwanamume fulani alikuwa akifanya kazi shambani na bila kutarajia akapata hazina iliyofichwa.

  •   Mfanyabiashara anayesafiri akitafuta lulu nzuri alipata lulu moja yenye thamani kubwa.

 Kwa hiari wanaume wote wawili waliuza vitu vyote walivyokuwa navyo ili wanunue hazina waliyoipata. Watu hawa wanawakilisha watu ambao wanathamini Ufalme hivi kwamba wanajidhabihu sana ili kupata baraka za Ufalme huo. (Luka 18:29, 30) Katika video hii, ona masimulizi ya watu wawili walio kama wanaume waliosimuliwa katika mifano hiyo miwili ya Yesu.