Georgia
Kwa kufaa, kuenea kwa ujumbe wa Ufalme nchini Georgia kunaonyeshwa kupitia mfano wa Yesu wa chachu iliyofichwa. (Mt. 13:33) Kama ilivyokuwa katika mfano wa chachu, ukuzi wa kiroho haukuonekana mwanzoni, lakini kwa muda mfupi ujumbe wa Ufalme ulianza kuenea sana na kubadili maisha ya wengi.
Soma kuhusu simulizi lenye kuchangamsha na kuchochea la upendo, imani, ushikamanifu, bidii, na ujasiri ulioonyeshwa na watu wa Mungu nchini Georgia “katika majira yanayofaa [na] katika majira yenye taabu.”—2 Tim. 4:2.
KATIKA SEHEMU HII
Maelezo Mafupi Kuhusu Georgia
Soma habari fupi kuhusu nchi, watu, tamaduni, na lugha ya pekee ya nchi hii iliyo karibu na Bahari Nyeusi.
Waliotafuta Kweli Zamani
Watu wenye uthamini waliojifunza kweli wakiwa maeneo mengine walikuja nchini Georgia na kuhubiri ujumbe wa Ufalme.
Mikutano Yawasaidia Wote Kukuza Imani
Mikutano ya Kikristo na machapisho ya Kigeorgia yaliwekaje msingi kwa ajili ya ukuzi uliofuata?
Nilitamani Sana Kubadili Maisha Yangu
Baada ya kumaliza utumishi wa kijeshi, Davit Samkharadze alisali apate msaada ili kuboresha maisha yake. Siku iliyofuata alikutana na Mashahidi wa Yehova.
Kutafuta Mwongozo wa Yehova
Tamazi Biblaia alitafuta na kupata msaada wa Mungu kabla ya kuhamia mji mwingine.
“Kwa Mungu Mambo Yote Yanawezekana”
Alipowasaidia Mashahidi wenzake kuchapisha machapisho ya Biblia katika Kigeorgia, Natela alikabili hali ambayo alifikiri ‘hawezi’ kukabiliana nayo.
Biblia ya Kigeorgia
Hati za kale za Biblia katika Kigeorgia ziliandikwa katika miaka ya 450 W.K. au hata mapema zaidi.
“Mungu Akaendelea Kuikuza.”—1 Kor. 3:6.
Baada ya nchi ya Georgia kupata uhuru, Mashahidi wa Yehova walifurahia ukuzi mkubwa wa kiroho.
Wachungaji Wenye Upendo Waandaa Mazoezi
Baada ya kuanguka kwa utawala wa Kikomunisti, Mashahidi walipangaje makutaniko, mikutano, makusanyiko, na utafsiri wa machapisho ya Biblia?
Mume Wangu Hakuweza Kuacha Kusoma!
Badri Kopaliani alikuwa na tamaa kubwa ya kusoma Biblia yake mpya, hivyo akachukua likizo kazini ili amalize kuisoma.
Mmekuwa Wapi Siku Hizo Zote?
Kabla ya mwaka kwisha baada ya kubatizwa, Artur Gerekhelia alihamia eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme.
Nilihisi Nimefanikiwa Maishani
Ingawa alikuwa na cheo cha juu katika Chama cha Kikomunisti nchini Georgia, Madona Kankia aliamua kufuatia mradi mwingine maishani.
Upendo wa Kweli wa Kikristo Haushindwi Kamwe
Wakati wa vita huko Abkhazia, Igor Ochigava na Gizo Narmania waliwasaidia Mashahidi wenzao kupata chakula na msaada wa kiroho.
Niliona kwa Macho Yangu Mwenyewe Kile Ambacho Biblia Inasema!
Kwa kuwa hakuwapenda Mashahidi wa Yehova, Pepo alifanya kile ambacho mama yake alimwambia: “Nenda ujionee mwenyewe mambo wanayofundisha.”
Baraka ‘Katika Majira Yanayofaa na Majira Yenye Taabu.’ —2 Tim. 4:2.
Idadi ya wahubiri iliongezeka kwa kasi sana katika miaka hiyo, kisha wimbi la upinzani likaanza kutoka chanzo ambacho hakikutarajiwa.
Vitisho Havikuwazuia Kumtumikia Yehova
Watu walitendaje Mashahidi wa Yehova walipotendewa kwa jeuri nchini Georgia?
“Hilo Ndilo Fungu la Urithi la Watumishi wa Yehova.”—Isa. 54:17.
Wahubiri wanaojitahidi kupanua utendaji wao wa kitheokrasi wanajionea baraka za Yehova.
Walimkumbuka Muumba Wao Mkuu
Asilimia 33 ya mapainia nchini Georgia wana umri usiozidi miaka 25.
Wakurdi Waikubali Kweli
Watu wanaomwogopa Mungu wanafurahi kusikia ujumbe wa kweli katika lugha yao wenyewe.
Upendo Unashinda Mipaka Iliyowekwa na Wanadamu
Akina nyanya (bibi) wawili walijionea upendo wa undugu wetu.