Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 9

Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia

Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia

“Mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia.”​—Ufunuo 14:7

Kama ulivyojifunza katika broshua hii, Biblia ina kanuni nyingi zinazoweza kukusaidia wewe na familia yako. Yehova anataka uwe na furaha. Anaahidi kwamba ukimtanguliza, ‘atakuongezea hivi vitu vingine vyote.’ (Mathayo 6:33) Yehova anataka uwe rafiki yake. Tumia kila fursa kusitawisha urafiki pamoja na Mungu. Hiyo ndiyo heshima kubwa zaidi ambayo mwanadamu anaweza kupata. ​—Mathayo 22:37, 38.

1 IMARISHA UHUSIANO WAKO NA YEHOVA

BIBLIA INASEMA HIVI: “‘Nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu,’ asema Yehova.” (2 Wakorintho 6:18) Mungu anataka uwe rafiki yake wa karibu. Sala ni njia moja ya kufanya hivyo. Yehova anakualika ‘usali bila kuacha.’ (1 Wathesalonike 5:17) Yeye yuko tayari kusikiliza mambo yanayokuhangaisha. (Wafilipi 4:6) Unaposali pamoja na familia yako, wataona jinsi unavyompenda Mungu.

Zaidi ya kuongea na Mungu unahitaji kumsikiliza. Unaweza kumsikiliza kwa kusoma Neno lake na machapisho yanayotegemea Biblia. (Zaburi 1:1, 2) Tafakari mambo unayojifunza. (Zaburi 77:11, 12) Kumsikiliza Mungu kunamaanisha pia kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida.​—Zaburi 122:1-4.

Kuwaeleza wengine kumhusu Yehova ni njia nyingine muhimu ya kuimarisha uhusiano wako naye. Kadiri unavyozidi kuwaeleza wengine kumhusu ndivyo unavyomkaribia zaidi Yehova.​—Mathayo 28:19, 20.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Tenga muda wa kusoma Biblia na kusali kila siku

  • Mkiwa familia, tangulizeni mambo ya kiroho badala ya burudani na vitumbuizo

2 FURAHIENI IBADA YENU YA FAMILIA

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Mnahitaji kupanga ratiba ya ibada ya familia na kuifuata. (Mwanzo 18:19) Lakini mengi yanahusika. Mungu anapaswa kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku. Imarisha uhusiano wa familia yako na Mungu kwa kuzungumza kumhusu “unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.” (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Uwe na lengo la kuiga mfano wa Yoshua, aliyesema hivi: “Mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.”​—Yoshua 24:15.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Panga ratiba ya kuendelea ambayo inazingatia mahitaji ya kila mshiriki wa familia