Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JenkoAtaman/stock.adobe.com

ENDELEA KUKESHA!

Sababu za Kuwa na Tumaini Katika 2023—Biblia Inasema Nini?

Sababu za Kuwa na Tumaini Katika 2023—Biblia Inasema Nini?

 Mwaka wa 2023 unapoanza sote tunatarajia mema kwa ajili yetu na familia zetu. Kwa nini tunaweza kuwa na tumaini?

Biblia inatoa tumaini

 Biblia inatoa habari njema kwamba matatizo tunayokabili sasa ni ya muda na kwamba hivi karibuni yatatuliwa. Kwa kweli, Biblia ‘iliandikwa ili kutufundisha, ili kupitia faraja kutoka kwa Maandiko tuwe na tumaini.’​—Waroma 15:4.

Tumaini linaloweza kukusaidia sasa

 Tumaini linalotajwa katika Biblia linaweza kuwa kama “nanga ya uhai wetu.” (Waebrania 6:19, maelezo ya chini) Tumaini hilo linaweza kutufanya tuwe imara. Linatusaidia kukabiliana na matatizo yetu ya sasa, kuwa na mtazamo mzuri, na kupata furaha ya kudumu. Kwa mfano:

  •   Ona jinsi tumaini la Biblia lilivyomsaidia mtu fulani aliyepambana na uraibu. Tazama video Nilichoshwa na Maisha Yangu.

  •   Ona jinsi tumaini la Biblia linavyoweza kutusaidia tunapompoteza mpendwa wetu katika kifo. Tazama video Faraja kwa Wanaoomboleza.

Imarisha tumaini lako

 Watu wengi wanatarajia kwamba mambo mema yatatendeka, lakini hawawezi kuwa na uhakika ikiwa matarajio yao yatatoshelezwa. Lakini ahadi za Biblia ni tofauti. Kwa nini? Kwa sababu ahadi za Biblia zinatoka kwa Yehova Mungu a mwenyewe, “asiyeweza kusema uwongo.” (Tito 1:2) Ni Yehova peke yake aliye na nguvu za kutimiza ahadi zake zote; anaweza kufanya “kila jambo apendalo.”​—Zaburi 135:5, 6.

 Tunakualika kwa uchangamfu unufaike kutokana na tumaini la Biblia linalotegemeka. Unaweza kujenga imani katika hilo tumaini kwa ‘kuyachunguza Maandiko kwa uangalifu.’ (Matendo 17:11) Jionee mwenyewe jambo hilo kwa kujaribu mtaala wetu wa kujifunza Biblia bila malipo. Anza mwaka wa 2023 ukiwa na tumaini!

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.