Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hizi Ni Nyakati za Hatari

Hizi Ni Nyakati za Hatari

Hizi Ni Nyakati za Hatari

BIBLIA ilitabiri kwamba wanadamu watapatwa na “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” Inafafanua kipindi hiki cha wakati kuwa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5; 2 Petro 3:3-7) Yesu Kristo alizungumzia kipindi hiki alipojibu swali aliloulizwa na wanafunzi wake kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3) Je, sasa tunaishi katika siku za mwisho? Linganisha kile ambacho Biblia ilitabiri na ripoti za hivi karibuni zilizonukuliwa hapa chini, kisha ujiamulie.

Biblia ilitabiri: vita vya ulimwenguni poteLuka 21:10; Ufunuo 6:4.

Ripoti za karibuni zinasema: “Katika karne ya 20, vifo vilivyotokana na vita vilikuwa mara tatu zaidi ya karne zote zilizopita zinapojumlishwa, tangu kuzaliwa kwa Kristo.”—Taasisi ya Worldwatch.

Biblia ilitabiri: upungufu wa chakula na magonjwaLuka 21:11; Ufunuo 6:5-8.

Ripoti za karibuni zinasema: Inakadiriwa kwamba mnamo 2004 watu milioni 863 duniani hawakuwa na chakula cha kutosha, hao ni watu milioni 7 zaidi ya mwaka wa 2003.—Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa.

Watu bilioni moja hivi wanaishi katika mitaa ya mabanda; watu bilioni 2.6 wanaishi katika maeneo yasiyo na mfumo wa kuondoa maji-taka na takataka; watu bilioni 1.1 hawana maji safi ya kunywa.—Taasisi ya Worldwatch.

Malaria huathiri watu milioni 500; watu milioni 40 wana UKIMWI; watu milioni 1.6 walikufa kwa sababu ya kifua kikuu mnamo 2005.—Shirika la Afya Ulimwenguni.

Biblia ilitabiri: kuharibiwa kwa dunia Ufunuo 11:18.

Ripoti za karibuni zinasema: “Shughuli za wanadamu zimetokeza uwezekano wa kutoweka kwa jamii nyingi za mimea na wanyama.” “Asilimia 60 hivi ya utendaji wa asili wa mifumo ya ikolojia ya dunia unaotegemeza uhai unapungua.”—Ukaguzi wa Milenia wa Mifumo ya Ikolojia.

“Gesi zinazoongeza joto ulimwenguni zinazotokezwa na wanadamu zinahatarisha hali ya hewa ya Dunia, na hivyo kufanya kuwe na uwezekano wa kuathiriwa vibaya kwa sayari hii.”—NASA, Taasisi ya Goddard ya Uchunguzi wa Angani.

Biblia ilitabiri: kuhubiriwa kwa habari njema za Ufalme wa Mungu duniani poteMathayo 24:14; Ufunuo 14:6, 7.

Ripoti za karibuni zinasema: Katika 2007, kilele cha Mashahidi wa Yehova 6,957,854 walitumia zaidi ya saa bilioni 1.4 wakihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika nchi 236.—Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2008.

Kama tulivyotangulia kutaja, Biblia ilitabiri kwamba ingawa kungekuwa na habari mbaya nyingi, kungekuwa na sababu ya kutarajia mema. Yesu alisema kungekuwa na “habari njema” ya Ufalme wa Mungu. Ufalme wa Mungu ni nini? Unawapa wanadamu tumaini la wakati ujao jinsi gani? Na Ufalme wa Mungu unakuhusu jinsi gani?

[Blabu katika ukurasa wa 5]

Biblia ilitabiri hali za ulimwengu tunazoona leo