Yona 3:1-10

  • Yona amtii Mungu na kwenda Ninawi (1-4)

  • Waninawi watubu baada ya kusikia ujumbe wa Yona (5-9)

  • Mungu aamua kutoangamiza Ninawi (10)

3  Ndipo neno la Yehova likamjia Yona mara ya pili likisema:+  “Inuka, nenda Ninawi+ lile jiji kubwa, ukalitangazie ujumbe ninaokuambia.”  Basi Yona akatii neno la Yehova,+ akainuka na kwenda Ninawi.+ Sasa Ninawi lilikuwa jiji kubwa sana*—mtu anayetembea kwa miguu angezunguka jiji hilo kwa siku tatu.  Ndipo Yona akaingia jijini, akatembea safari ya siku moja akitangaza hivi: “Bado siku 40 tu, jiji la Ninawi litaangamizwa.”  Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu,+ nao wakatangaza watu wafunge na kuvaa magunia, kuanzia aliye mkubwa zaidi hadi aliye mdogo zaidi.  Ujumbe huo ulipomfikia mfalme wa Ninawi, aliinuka kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua vazi lake la kifalme, akavaa nguo za magunia, na kuketi katika majivu.  Pia, akaamuru tangazo hili litolewe katika jiji lote la Ninawi: “Kwa agizo la mfalme na wakuu wake: Hakuna mwanadamu yeyote wala mnyama yeyote wa kufugwa anayepaswa kula kitu chochote. Hawapaswi kula chakula wala hawapaswi kunywa maji.  Wote wavae magunia, mwanadamu na mnyama; na wamwite Mungu kwa bidii na kuacha njia zao ovu na matendo yao ya ukatili.  Ni nani anayejua ikiwa Mungu wa kweli hatafikiria upya* jambo analokusudia kufanya na kuacha hasira yake inayowaka, ili tusiangamie?” 10  Mungu wa kweli alipoona waliyofanya, jinsi walivyoacha njia zao ovu,+ akafikiria upya kuhusu* msiba aliosema kwamba angewaletea, naye hakuuleta.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “jiji kubwa mbele za Mungu.”
Au “hataghairi kuhusu.”
Au “akaghairi kuhusu.”