Mambo ya Walawi 23:1-44

  • Siku takatifu na sherehe takatifu (1-44)

    • Sabato (3)

    • Pasaka (4, 5)(4, 5)

    • Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu (6-8)

    • Kutoa mazao au matunda ya kwanza (9-14)

    • Sherehe ya Majuma (15-21)

    • Njia inayofaa ya kuvuna (22)

    • Sherehe ya Kupiga Tarumbeta (23-25)

    • Siku ya Kufunika Dhambi (26-32)

    • Sherehe ya Vibanda (33-43)

23  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Waambie hivi Waisraeli: ‘Sherehe za Yehova za majira+ ambazo mnapaswa kutangaza+ ni makusanyiko matakatifu. Hizi ndizo sherehe zangu za majira:  “‘Mnaweza kufanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba ni sabato ya pumziko kamili,+ kusanyiko takatifu. Hamtafanya kazi yoyote. Ni sabato kwa Yehova popote mnapoishi.+  “‘Hizi ndizo sherehe za Yehova za majira, makusanyiko matakatifu ambayo mnapaswa kutangaza katika nyakati zilizopangwa za sherehe hizo:  Katika siku ya 14 ya mwezi wa kwanza,+ wakati wa jioni kabla ya giza kuingia* ni Pasaka+ ya Yehova.  “‘Siku ya 15 ya mwezi huo ni Sherehe ya Yehova ya Mikate Isiyo na Chachu.+ Kwa siku saba mnapaswa kula mikate isiyo na chachu.+  Siku ya kwanza, mtakuwa na kusanyiko takatifu.+ Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.  Lakini kwa siku saba mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Siku ya saba kutakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.’”  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 10  “Waambie hivi Waisraeli: ‘Hatimaye mtakapoingia katika nchi ninayowapa na kuvuna mazao yake, ni lazima mumletee kuhani tita la mavuno yenu ya kwanza.+ 11  Naye kuhani atatikisa tita hilo mbele za Yehova kwenda mbele na nyuma ili mpate kibali. Atalitikisa siku inayofuata siku ya Sabato. 12  Siku ambayo tita hilo linatikiswa, ni lazima mumtolee Yehova dhabihu ya kuteketezwa ya mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiye na kasoro. 13  Mtatoa pia sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa* ya unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka linalochomwa kwa moto, lenye harufu inayompendeza* Yehova. Pia mtatoa robo ya hini* ya divai kuwa toleo la kinywaji. 14  Msile mkate wowote, nafaka zilizokaangwa, au nafaka zilizotoka kuvunwa, mpaka mtakapomtolea Mungu dhabihu zenu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote mahali popote mtakapoishi. 15  “‘Mnapaswa kuhesabu sabato saba kuanzia siku inayofuata siku ya Sabato, siku mnayotoa tita la toleo la kutikiswa.+ Yanapaswa kuwa majuma kamili. 16  Mtahesabu siku 50+ mpaka siku inayofuata Sabato ya saba, kisha mtamtolea Yehova toleo la nafaka iliyotoka kuvunwa.+ 17  Mnapaswa kuleta mikate miwili kutoka nyumbani ili iwe toleo la kutikiswa. Mikate hiyo inapaswa kuokwa kwa kutumia sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa* ya unga laini. Inapaswa kuwa na chachu,+ ni mazao ya kwanza yaliyokomaa yanayotolewa kwa Yehova.+ 18  Nanyi mnapaswa kutoa mikate hiyo pamoja na wanakondoo dume saba wa mwaka mmoja wasio na kasoro, ng’ombe dume mmoja mchanga, na kondoo dume wawili.+ Watatolewa kwa Yehova wakiwa dhabihu ya kuteketezwa pamoja na toleo la nafaka na matoleo ya vinywaji, dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova. 19  Pia mnapaswa kumtoa mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi+ na wanakondoo dume wawili wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya ushirika.+ 20  Kuhani atazitikisa dhabihu hizo kwenda mbele na nyuma pamoja na ile mikate ya mazao ya kwanza yaliyokomaa kama dhabihu ya kutikiswa mbele za Yehova, pamoja na wale wanakondoo dume wawili. Ni vitu vitakatifu vinavyotolewa kwa Yehova kwa ajili ya kuhani.+ 21  Siku hiyo mtatangaza+ na kufanya kusanyiko takatifu. Hamtafanya kazi yoyote ngumu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote mahali popote mnapoishi. 22  “‘Mnapovuna mashamba yenu, msivune kabisa ukingo wa mashamba yenu, nanyi msiokote masalio ya mavuno yenu.+ Waachieni maskini*+ na wageni.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’” 23  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 24  “Waambie hivi Waisraeli: ‘Siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mtakuwa na pumziko kamili, mtaadhimisha kusanyiko takatifu litakalotangazwa kwa mlio wa tarumbeta.+ 25  Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu, nanyi mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto.’” 26  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 27  “Hata hivyo, siku ya kumi ya mwezi huo wa saba ni Siku ya Kufunika Dhambi.+ Mtakuwa na kusanyiko takatifu, nanyi mnapaswa kujitesa*+ na kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. 28  Hampaswi kufanya kazi yoyote siku hiyo kwa sababu ni siku ya kufunika dhambi+ zenu mbele za Yehova Mungu wenu. 29  Mtu yeyote ambaye hatajitesa* siku hiyo atauawa.+ 30  Nami nitamwangamiza mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo. 31  Hampaswi kufanya kazi yoyote. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote mahali popote mtakapoishi. 32  Ni sabato ya pumziko kamili kwenu, nanyi mtajitesa+ siku ya tisa ya mwezi huo wakati wa jioni. Mtaadhimisha sabato kuanzia jioni hiyo mpaka jioni inayofuata.” 33  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 34  “Waambie hivi Waisraeli: ‘Siku ya 15 ya mwezi huo wa saba mtamfanyia Yehova Sherehe ya Vibanda* kwa siku saba.+ 35  Mtakuwa na kusanyiko takatifu siku ya kwanza, nanyi hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu. 36  Kwa siku saba mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Ni kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu. 37  “‘Hizo ndizo sherehe za Yehova za majira+ mnazopaswa kutangaza kuwa makusanyiko matakatifu+ ya kumtolea Yehova dhabihu hizi zinazochomwa moto: dhabihu ya kuteketezwa+ pamoja na toleo lake la nafaka+ na matoleo ya vinywaji+ kulingana na ratiba ya kila siku. 38  Mtazitoa pamoja na dhabihu zinazotolewa wakati wa sabato za Yehova,+ pamoja na zawadi zenu,+ dhabihu zenu za nadhiri,+ na matoleo yenu ya hiari+ ambayo mnapaswa kumtolea Yehova. 39  Hata hivyo, siku ya 15 ya mwezi wa saba, baada ya kukusanya mavuno yenu, mnapaswa kufanya sherehe ya Yehova kwa siku saba.+ Siku ya kwanza ni ya pumziko kamili na siku ya nane ni ya pumziko kamili.+ 40  Siku ya kwanza, mtachukua matunda ya miti yenu bora, matawi ya mitende,+ matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bondeni, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu kwa siku saba.+ 41  Mtamfanyia Yehova sherehe hiyo kwa siku saba kila mwaka.+ Kwa kuwa ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote, mnapaswa kuisherehekea katika mwezi wa saba. 42  Mtakaa katika vibanda kwa siku saba.+ Waisraeli wote watakaa katika vibanda, 43  ili vizazi vyenu vinavyokuja vijue kwamba+ niliwafanya Waisraeli wakae katika vibanda nilipowatoa nchini Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’” 44  Basi Musa akawaambia Waisraeli kuhusu sherehe za Yehova za majira.

Maelezo ya Chini

Tnn., “katikati ya zile jioni mbili.”
Hini ilikuwa sawa na lita 3.67. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”
Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na lita 4.4 au kilogramu 2.6 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na lita 4.4 au kilogramu 2.6 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”
Au “wanaoteseka.”
Kwa ujumla inaeleweka kwamba “kujitesa” kunamaanisha kujinyima kwa njia mbalimbali, kutia ndani kufunga.
Au labda, “hatafunga.”
Au “Vibanda vya Muda.”