Barua ya Pili kwa Wakorintho 4:1-18

  • Nuru ya habari njema (1-6)

    • Akili za wasioamini zimepofushwa (4)

  • Hazina katika vyombo vya udongo (7-18)

4  Kwa hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii kupitia rehema tuliyoonyeshwa, hatufi moyo.  Hata hivyo, tumeyakataa mambo ya kichinichini ya aibu, hatutembei kwa ujanja, au kulichanganya na kitu chochote neno la Mungu;+ bali kwa kufanya kweli iwe wazi, tunajipendekeza kwa kila dhamiri ya mwanadamu machoni pa Mungu.+  Ikiwa kwa kweli habari njema tunayotangaza imefunikwa kwa kitambaa, imefunikwa kati ya wale wanaoangamia,  ambao kati yao mungu wa mfumo huu wa mambo*+ amezipofusha akili za wasioamini,+ ili nuru ya* habari njema yenye utukufu kuhusu Kristo, aliye mfano wa Mungu,+ isiwaangazie.+  Kwa maana tunahubiri, si kuhusu sisi wenyewe, bali kuhusu Yesu Kristo kwamba ni Bwana na sisi wenyewe kwamba ni watumwa wenu kwa ajili ya Yesu.  Kwa maana Mungu ndiye aliyesema: “Nuru na iangaze kutoka katika giza,”+ naye ameangaza juu ya mioyo yetu ili kuimulika+ kwa ujuzi wenye utukufu kumhusu Mungu kupitia uso wa Kristo.  Hata hivyo, tuna hazina hii+ katika vyombo vya udongo,*+ ili nguvu zinazopita zile za kawaida ziwe za Mungu na si kutoka kwetu.+  Tunakandamizwa katika kila njia, lakini hatubanwi kupita kiasi cha kushindwa kusonga; tunafadhaishwa, lakini si bila njia ya kutokea kabisa;*+  tunateswa, lakini hatuachwi bila msaada;+ tunaangushwa chini, lakini hatuangamizwi.+ 10  Sikuzote katika mwili wetu tunavumilia matendo yenye kuleta kifo ambayo Yesu aliteseka,+ ili uzima wa Yesu ufunuliwe pia katika mwili wetu. 11  Kwa maana sikuzote sisi tunaoishi tunakabili kifo uso kwa uso+ kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu ufunuliwe pia katika mwili wetu unaoweza kufa. 12  Kwa hiyo kifo kinafanya kazi ndani yetu, lakini uzima ndani yenu. 13  Basi kwa sababu tuna roho ileile ya imani kama ile iliyoandikwa hivi kuihusu: “Mimi nilionyesha imani, kwa hiyo nikasema”;+ sisi pia tunaonyesha imani na kwa hiyo tunasema, 14  tukijua kwamba Yule aliyemfufua Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu naye atatutokeza sisi pamoja nanyi.+ 15  Kwa maana mambo yote haya ni kwa ajili yenu, ili fadhili zisizostahiliwa zinazoongezeka zizidi kuwa nyingi kwa sababu wengi zaidi wanatoa shukrani kwa utukufu wa Mungu.+ 16  Kwa hiyo, hatufi moyo, lakini hata ikiwa mtu tuliye kwa nje anachakaa, hakika mtu tuliye kwa ndani anafanywa upya siku kwa siku. 17  Kwa maana ingawa dhiki* ni ya muda mfupi na ni nyepesi, inatokeza kwa ajili yetu utukufu ulio mkuu* na bora zaidi na zaidi, na wa milele;+ 18  huku tukikaza macho yetu, si juu ya vitu vinavyoonekana, bali juu ya vitu visivyoonekana.+ Kwa maana vitu vinavyoonekana ni vya muda, lakini vitu visivyoonekana ni vya milele.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “mwangaza wa.”
Au “katika mitungi ya udongo.”
Au labda, “tukiwa tumekata tamaa.”
Au “majaribu.”
Tnn., “ulio na uzito.”