Barua ya Kwanza kwa Timotheo 3:1-16

  • Sifa za kustahili kuwa waangalizi (1-7)

  • Sifa za kustahili kuwa watumishi wa huduma (8-13)

  • Siri takatifu ya ujitoaji-kimungu (14-16)

3  Maneno haya ni yenye kutegemeka: Ikiwa mwanamume anajitahidi kuwa mwangalizi,+ anatamani kazi njema.  Mwangalizi anapaswa kuwa mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi katika mazoea, mwenye utimamu wa akili,*+ mwenye utaratibu, mkaribishaji wageni,*+ mwenye uwezo wa kufundisha,+  si mlevi,+ si mkatili,* bali mwenye usawaziko,+ si mgomvi,+ si mtu anayependa pesa,+  mwanamume anayeisimamia* nyumba yake vizuri, mwenye watoto wanaojitiisha na kuchukua mambo kwa uzito+  (kwa maana ikiwa mtu hajui jinsi ya kuisimamia* nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?),  si mtu aliyegeuka hivi karibuni,+ ili asije akawa na kiburi na kuanguka katika hukumu aliyohukumiwa Ibilisi.  Pia, anapaswa kushuhudiwa vema na* watu walio nje+ ili asianguke katika shutuma* na mtego wa Ibilisi.  Vilevile watumishi wa huduma wanapaswa kuchukua mambo kwa uzito, si wenye ndimi mbili,* si wenye kunywa divai nyingi, si wenye pupa ya mapato yasiyo ya haki,+  wakiishika siri takatifu ya imani kwa dhamiri safi.+ 10  Pia, wanapaswa kwanza kujaribiwa* kama wanafaa; ndipo watumike wakiwa wahudumu, kwa kuwa hawana shtaka.+ 11  Vilevile wanawake wanapaswa kuchukua mambo kwa uzito, wasiwe wachongezi,+ wawe wenye kiasi katika mazoea, na waaminifu katika mambo yote.+ 12  Watumishi wa huduma wanapaswa kuwa waume wa mke mmoja, wanaosimamia vizuri watoto wao na nyumba zao wenyewe. 13  Kwa maana wanaume wanaohudumu vizuri wanajipatia sifa nzuri na uhuru mwingi wa kusema katika imani iliyo katika Kristo Yesu. 14  Ninakuandikia mambo haya, ingawa ninatumaini kuja kwako upesi, 15  ili nikichelewa ujue jinsi unavyopaswa kutenda katika nyumba ya Mungu,+ ambayo ni kutaniko la Mungu aliye hai, nguzo na tegemezo la ile kweli. 16  Kwa kweli, siri takatifu ya huu ujitoaji-kimungu* ni kubwa: ‘Alifunuliwa katika mwili,+ alitangazwa kuwa mwadilifu katika roho,+ aliwatokea malaika,+ alihubiriwa kati ya mataifa,+ watu walimwamini ulimwenguni,+ akapokewa mbinguni kwa utukufu.’

Maelezo ya Chini

Au “anayefanya maamuzi mazuri; mwenye busara.”
Au “mkarimu.”
Au “mtu anayepiga watu.”
Au “anayeongoza.”
Au “kuongoza.”
Au “asipate aibu.”
Au “kuwa na sifa nzuri kutoka kwa”
Au “waseme kwa unyoofu.”
Au “wajaribiwe kama wanastahili.”
Angalia Kamusi.