Hamia kwenye habari

Ni Nini Maana ya Uhai?

Ni Nini Maana ya Uhai?

Jibu la Biblia

 Swali kuhusu maana ya uhai linaweza kuulizwa katika njia nyingi, kama vile, Kwa nini tuko hapa? au Je, maisha yana kusudi? Biblia inaonyesha kwamba kusudi letu maishani ni kujenga uhusiano mzuri pamoja na Mungu. Fikiria baadhi ya kweli za msingi zifuatazo ambazo Biblia hufunua.

  •   Mungu ni Muumba wetu. Biblia inasema: “Yeye [Mungu] ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.”​—Zaburi 100:3; Ufunuo 4:11.

  •   Mungu ana kusudi kuhusu kila kitu anachoumba, kutia ndani sisi wenyewe.​—Isaya 45:18.

  •   Mungu alituumba tukiwa na “uhitaji kwa kiroho,” unaotia ndani tamaa ya kuwa na maisha yenye kusudi. (Mathayo 5:3) Anataka tutosheleze tamaa hiyo.​—Zaburi 145:16.

  •   Tunatosheleza uhitaji wetu wa kiroho kwa kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Ingawa, huenda wengine wakafikiri kwamba haiwezekani kuwa rafiki za Mungu, Biblia inatutia Moyo: ‘Tumkaribie Mungu, naye atatukaribia.’​—Yakobo 4:8; 2:23.

  •   Ili kuwa rafiki za Mungu, lazima tuishi kupatana na kusudi lake kutuelekea. Biblia inazungumzia jambo hilo kwenye andiko la Mhubiri 12:13: “Mche Mungu, na uzishike amri zake, kwa sababu hilo ndilo jukumu aliloumbiwa binadamu.”​—Biblia Habari Njema.

  •   Wakati ujao, tutajionea wenyewe kusudi halisi la maisha atakapoondoa kuteseka na kuwapatia uzima wa Milele, wale wote wanaomwabudu.​—Zaburi 37:10, 11.