Hamia kwenye habari

Kwa Nini Nisali? Je, Mungu Atanijibu?

Kwa Nini Nisali? Je, Mungu Atanijibu?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, atajibu. Biblia na pia masimulizi ya watu yanaonyesha kwamba Mungu hujibu sala. Biblia inasema: “[Mungu] atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao, naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.” (Zaburi 145:19) Ili Mungu ajibu sala zako inategemea kwa kiasi kikubwa wewe.

Mambo yaliyo muhimu kwa Mungu

  •   Tunapaswa kusali kwa Mungu na si kwa Yesu, Maria, watakatifu, malaika, au sanamu. Yehova Mungu peke yake ndiye “msikiaji wa sala.”​—Zaburi 65:2.

  •   Tunapaswa kusali kupatana na mapenzi au matakwa ya Mungu yanayopatikana katika Biblia.​—1 Yohana 5:14.

  •   Tunapaswa kusali katika jina la Yesu, na hivyo kutambua mamlaka yake. Yesu alisema: “Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.”—Yohana 14:6.

  •   Tunapaswa kusali kwa imani, tukiomba imani zaidi ikiwa tunaihitaji.​— Mathayo 21:22; Luka 17:5.

  •   Tunapaswa kuwa wanyenyekevu na wanyofu. Biblia inasema: “Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu.”​—Zaburi 138:6.

  •   Tunapaswa kusali bila kuacha. Yesu alisema: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa.”​—Luka 11:9.

Mambo yasiyo muhimu kwa Mungu

  •   Rangi au taifa lako. “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”​—Matendo 10:34, 35.

  •   Kikao chako unaposali. Unaweza kusali kwa Mungu ukiwa umeketi, umeinama chini, umepiga magoti, au umesimama.​—1 Mambo ya Nyakati 17:16; Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25.

  •   Iwe unasali kwa sauti au kimyakimya. Mungu hujibu hata sala za kimyakimya ambazo watu wengine hawasikii.​—Nehemia 2:1-6.

  •   Iwe mahangaiko yako ni makubwa au madogo. Mungu anakutia moyo ‘umtupie mahangaiko yako yote juu yake, kwa sababu yeye anakujali wewe.’​—1 Petro 5:7.