Hamia kwenye habari

Mashahidi wa Yehova wakitoa machapisho yanayotegemea Biblia katika michezo iliyofanywa karibuni nchini Ekuado

DESEMBA 26, 2022
EKUADO

Mahubiri ya Hadharani Yawafikia Maelfu Nchini Ekuado

Mahubiri ya Hadharani Yawafikia Maelfu Nchini Ekuado

Oktoba 29, 2022, fainali ya shindano la timu bora zaidi za mpira Amerika Kusini linaloitwa Copa Libertadores ilifanyika jijini Guayaquil, Ekuado. Mashahidi 1,500 wa Yehova walitangaza habari njema kwa kutumia vigari siku kadhaa kabla na baada ya tukio hilo muhimu.

Akina ndugu waliweka vigari 135 katika maeneo 45 jijini yenye watu wengi. Ndugu na dada wengi walirekebisha ratiba zao ili washiriki katika mahubiri hayo ya pekee. Kulikuwa na maelfu ya wageni kutoka Brazili kwa hiyo baadhi ya ndugu na dada zetu waliamua kujifunza maneno machache ya Kireno ili kuwavutia watalii hao.

Waliwahubiria watu wengi sana. Kwa mfano, wahubiri walitoa machapisho 796 ndani ya siku moja tu. Kufikia Novemba 2, Mashahidi walikuwa wametoa jumla ya machapisho 5,139 katika mahubiri hayo ambayo yalifanywa kwa siku kumi.

Ndugu Davide del Monte, ambaye alisaidia kusimamia kazi hiyo, alisema: “Watalii wengi walijihisi huru kupiga picha kwa sababu ndugu na dada waliokuwa kwenye vigari walikuwa wenye fadhili na waliwakaribisha kwa kutabasamu. Watalii wengine waliwapongeza akina ndugu na dada kwa kuwa na utaratibu na kwa kuvalia vizuri, na pia walitaja kwamba machapisho yetu ni muhimu sana.”

Mwanamke mmoja aliyekuja kwenye kigari alisema: “Niliwatambua kutoka mbali. Mnaongea bila kusema neno lolote. Mna mpango mzuri sana.”

Ni wazi kwamba jitihada hizo za kutoa ushahidi zimemletea sifa Yehova kwa sababu hekima yake inaendelea “kuinua sauti yake katika viwanja vya jiji” na “kwenye makutano ya barabara zenye watu wengi.”​—Methali 1:20, 21.