Ona video zinazopatikana

Funzo Moja Ilileta Mafunzo Mingi

Funzo Moja Ilileta Mafunzo Mingi

 Marta, dada moja Shahidi wa Yehova mwenye kuishi Guatemala, anajifunza luga ya Kekchi ili aweze kufundisha Biblia watu wenye wanasema ile luga. Siku moja, aliona mwanaume fulani mwenye alikuwa anatoka mu hopitali. Kisha kuangalia manguo ya ule mwanaume, dada yetu aliona kama ule mwanaume alipaswa tu kuwa mutu mwenye anaishi mu kijiji ya Kekchi, katika eneo yenye milima-milima, fasi kwenye Mashahidi hawajahubiri sana. Alimusogelea na akamusemesha akitumia maneno fulani yenye alikuwa anajua mu luga ya Kekchi.

 Marta alimuomba aanze kujifunza naye Biblia. Ule mwanaume alikubali kwa furaha, lakini akasema kama hana makuta ya kulipa ile mafundisho ya Biblia. Marta akamufasiria kama Mashahidi wa Yehova wanafundishaka watu Biblia bila malipo. Dada akamuambia kama yeye na familia yake wanaweza kufuata mafundisho kupitia telefone yake. Ule mwanaume akakubali. Kwa kuwa ule mwanaume alijua kusoma luga ya Kiespagnol, Marta alimupatia Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Kiespagnol, na kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? ya luga ya Kekchi. Juma yenye ilifuata, ule mwanaume, bibi yake na watoto wao wawili walianza kujifunza Biblia na dada Marta kupitia telefone. Walikuwa wanajifunza mara mbili kwa juma. Marta anaeleza hivi: “Juu sikukuwa najua muzuri luga ya Kekchi, funzo ilikuwa inafanyika mu luga ya Kiespagnol, kisha baba alikuwa anafasiria bibi yake mu luga ya kekchi. Watoto walikuwa wanaelewa Kiespagnol.”

 Ule mwanaume alikuwa pastere mu kanisa yake. Alianza kufundisha watu wa kanisa yake mambo yote yenye alikuwa anajifunza mu Biblia. Watu wa kanisa yake walifurahia sana ile mafundisho na wakamuuliza ni wapi alipata ile mafundisho ya mupya. Wakati aliwaelezea juu ya funzo yake ya Biblia, wote wakaanza kuja ku funzo, mumoja kisha mwingine. Kisha siku kidogo, watu 15 hivi walianza kuhuzuria ku funzo ili wajifunze na dada Matra kupitia telefone. Juu kila mutu asikie muzuri, micro ilitiwa karibu na telefone.

 Wakati Marta alizungumuza na wazee wa kutaniko yake kuhusu ile funzo yake ya Biblia, mumoja wao alienda mu ile kijiji, kwenye wale wanafunzi walikuwa wanaishi. Aliwaalika ili wakuje kusikiliza hotuba yenye mwangalizi wa muzunguko * angetoa mu kijiji ingine. Juu ya kufika ku ile kijiji ili kusikiliza hotuba, iliomba kufanya saa mbili mu gari, kisha tena saa mbili za kutembea na miguu. Wale wanafunzi walikubali kuenda mwa ile eneo ingine, na walikuwa 17 ili kusikiliza hotuba.

 Kisha majuma fulani, mwangalizi pamoja na Mashahidi wengine walifanya siku ine pamoja na wale wanafunzi. Kila asubui, walikuwa wanaangalia video za luga ya Kekchi ku JW.ORG na walikuwa wanajifunza broshua Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo? Kisha midi walikuwa wanaangalia programu za JW Télédiffusion. Mwangalizi alichukua mipango ili kila mumoja wa wanafunzi apate funzo ya Biblia yake mwenyewe.

 Mu zile siku ine, Mashahidi wa Yehova walihubiri mu maeneo jirani yenye kuzungumuza luga ya Kekchi na wakaalika wakaaji wa ile maeneo ku mukutano wa pekee. Ku ile mukutano, ndugu zetu waliomba watu 47 wenye walikuja kama wanaweza kukubali kuanza kujifunza Biblia. Familia 11 zilikubali.

 Kisha miezi fulani, wazee walichukua mipango ili kila mwisho wa juma, mukutano ufanyike mu kijiji ya ule mwanaume mwenye alianzaka funzo wa kwanza. Leo watu 40 hivi wanahuzuria mikutano kwa ukawaida. Na wakati ndugu walifanya Ukumbusho wa kifo cha Yesu mu ile kijiji, watu 91 walihuzuria.

 Wakati anakumbuka vile mambo ilianzaka na kuendelea, Marta anasema: “Namushukuru Yehova. Wakati fulani naonaka sawa vile siwezi kufanya kitu ya maana. Lakini, siye ni vyombo tu ndani ya mikono ya Yehova. Alielewa ni nini ilikuwa ndani ya mioyo ya watu wa ile eneo, na aliwavuta kwa watu wake. Yehova anawapenda.”

^ Mwangalizi wa muzunguko ni muzee mwenye ni Shahidi wa Yehova mwenye anatembeleaka makutaniko 20 hivi yenye inafanyiza muzunguko moja.