Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 9

Mumuabudu Yehova Katika Familia

Mumuabudu Yehova Katika Familia

‘Mumuabudu yeye aliyezifanya mbingu na dunia.’​—Ufunuo 14:7

Umejifunza katika broshua hii kwamba Biblia ina kanuni nyingi ambazo zitakusaidia wewe na familia yako. Yehova anataka muwe na furaha. Anaahidi kwamba ikiwa munatia ibada yake pa nafasi ya kwanza, ‘mutaongezewa hivi vitu vingine vyote.’ (Mathayo 6:33) Kwa kweli, anataka muwe rafiki zake. Mufaidike na kila nafasi inayojitokeza ili kukomalisha urafiki wenu naye. Hilo ndilo pendeleo kubwa zaidi ambalo mutu anaweza kuwa nalo.​—Mathayo 22:37, 38.

1 MUKOMALISHE URAFIKI WENU NA YEHOVA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: Yehova anatuambia hivi: ‘Nitakuwa baba kwenu, nanyi mutakuwa wana na mabinti kwangu.’ (2 Wakorintho 6:18) Mungu anataka muwe rafiki zake wa karibu. Sala ni njia moja ya kumukaribia. Yehova anatuomba ‘tusali bila kuacha.’ (1 Wathesalonike 5:17) Iko tayari kukusiliza unapomuelezea mawazo yako ya ndani na mahangaiko yako. (Wafilipi 4:6) Wakati unasali pamoja na familia yako, wataona ni kwa kadiri gani Mungu iko halisi kwako.

Zaidi ya kuzungumuza na Mungu katika sala, ni lazima kumusikiliza. Unaweza kumusikiliza kwa kujifunza Neno lake Biblia na vichapo vinavyotegemea Biblia. (Zaburi 1:1, 2) Tafakari juu ya mambo ambayo unajifunza. (Zaburi 77:11, 12) Tena, ili kumusikiliza Mungu, ni lazima kuhuzuria mikutano kwa ukawaida.​—Zaburi 122:1-4.

Kuwaelezea wengine kuhusu Yehova ni njia nyingine ya maana ya kufanya urafiki wetu naye ukomae. Kadiri tunawaelezea wengine kumuhusu, ndivyo tunamukaribia zaidi.​—Mathayo 28:19, 20.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Panga wakati wa kujifunza Biblia na kusali kila siku

  • Mukiwa familia, muhangaikie kwanza mambo ya kiroho kuliko mambo ya kujifurahisa

2 MUFURAHIE IBADA YENU YA FAMILIA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ (Yakobo 4:8) Ni vizuri kupanga programu ya ibada ya familia ya kila juma na kuifanya kwa ukawaida. (Mwanzo 18:19) Lakini hiyo haitoshe. Ni lazima mumupatie Mungu nafasi katika maisha yenu ya kila siku. Mukomalishe uhusiano wenu na Yehova kwa kuzungumuza kumuhusu ‘munapoketi katika nyumba yenu na munapotembea barabarani na munapolala na munapoamuka.’ (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Muazimie kumuiga Yoshua, ambaye alisema hivi: ‘Lakini mimi na nyumba yangu, tutamutumikia Yehova.’​—Yoshua 24:15.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Muwe na ibada ya familia inayofanywa kwa ukawaida na ambayo inafikiria mahitaji ya kila mushiriki wa familia