Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Urusi Inashambulia Ukraine

Urusi Inashambulia Ukraine

 Asubui-asubui ya siku ya Tano, tarehe 24, Mwezi wa 2, 2022, majeshi ya Urusi ilianza kuingia Ukraine, hata kama viongozi wa inchi mbalimbali walijikaza sana juu ya kuepuka vita. Ile mapambano ya kijeshi inaweza kuwa na matokeo gani mu dunia? António Guterres, Sekretere Mukubwa wa Umoja wa Mataifa, alisema hivi masiku fulani yenye imepita: “Mateso yenye watu wanaweza kupata, uharibifu, na kupotea kwa amani mu Ulaya na mu dunia yote, ni tatizo kubwa sana yenye hatupendi kufikia.”

Kulingana na Biblia, matukio sawa ile iko na maana gani?

  •   Yesu Kristo alitabiri wakati wenye “taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.” (Matayo 24:7) Soma habari “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?” juu uone namna Biblia inaonyesha kama vita zenye kutokea leo zinatimiza unabii wa Yesu.

  •   Kitabu ya Ufunuo yenye kuwa mu Biblia inafananisha vita na mupandaji-farasi mwenye anaikala ku “farasi mwenye rangi ya moto” na mwenye anatosha “amani katika dunia.” (Ufunuo 6:4) Soma habari “Wale Wapanda-Farasi Ine​—Ni Nani?” juu uone namna ule unabii unahusu vita za leo.

  •   Kitabu ya Danieli ilitabiri ushindani kati ya “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini.” (Danieli 11:25-45) Angalia video Unabii Wenye Umetimia​—Danieli Sura ya 11 ili ujue juu ya nini tunaweza kusema kama Urusi na inchi zenye kuiunga mukono njo mufalme wa kaskazini. a

  •   Ufunuo inazungumuzia pia “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Lakini hii haiko vita kati ya mataifa sawa ile yenye tuko naona leo. Soma habari “Vita ya Har-Magedoni Ni Nini?” juu upate habari zaidi kuhusu ile tukio yenye itatokea wakati wenye kuya.

Juu ya nini tunaweza kutumaini kama mambo itakuwa muzuri wakati wenye kuya?

  •   Biblia inasema kama Mungu atamaliza “vita katika dunia yote.” (Zaburi 46:9) Soma habari “Tumaini Bora la Wakati Ujao” ili ujue mambo mingi zaidi juu ya mambo ya muzuri yenye Mungu atatufanyia mu siku zenye ziko nakuya.

  •   Yesu alifundisha wanafunzi wake wasali juu Ufalme wa Mungu ukuye. (Matayo 6:9, 10) Ile Ufalme ni serikali ya mbinguni yenye itatimiza mapenzi ya Mungu ku dunia. Na kuleta amani mu dunia, ni kati ya mapenzi ya Mungu. Juu ya kujua faida zenye Ufalme wa Mungu unaweza kukuletea, angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini?

 Mashahidi wa Yehova zaidi ya 129 000 wanaishi mu Ukraine. Sawa vile Mashahidi wengine wa mu inchi zingine, wao pia wanatii Yesu kwa kukatala kujiingiza mu mambo ya politike na kukatala kujiingiza mu vita. (Yohana 18:36) Mu dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanaendelea kutangaza “habari njema ya Ufalme” na kuonyesha kama ile Ufalme tu njo itamaliza magumu yote ya wanadamu, sawa vile vita. (Matayo 24:14) Tunakuomba ututafute juu ujifunze mambo mingi zaidi kuhusu tumaini yenye Biblia inatupatia.

a Juu upate maelezo zaidi kuhusu hii unabi, ona habari “‘Mufalme wa Kaskazini’ Katika Wakati wa Mwisho” na “Ni Nani ‘Mufalme wa Kaskazini’ Leo?