Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Kweli Yesu alifufua watu?

Yesu alifufua Lazaro, aliyekuwa amefanya siku ine katika kaburi

Biblia inasema waziwazi kama Yesu alifufua watu waliokuwa wamekufa. Habari hizo haziko za kuwazia tu; mambo hayo yalifanyika mahali na wakati wa kweli. Kwa mufano, wakati wa kiangazi cha mwaka wa 31, kikundi kikubwa cha watu kilisafiri pamoja na Yesu kutoka Kapernaumu mupaka Naini. Walipofika huko, walikutana na kikundi kingine. Unaweza kuamini habari ya ufufuo uliofanywa kisha hapo kwa sababu inaandikwa katika Neno la Mungu, Biblia, na kwa sababu ufufuo huo ulifanywa mbele ya mashahidi hao wote.—Soma Luka 7:11-15.

Yesu alifufua pia rafiki yake Lazaro, aliyekuwa amefanya siku ine katika kaburi. Unaweza kuamini habari juu ya jambo Yesu alifanya siku hiyo kwa sababu jambo hilo pia lilionwa na mashahidi wengi.—Soma Yohana 11:39-45.

Sababu gani Yesu alifufua watu?

Yesu alifufua watu kwa sababu alichochewa na huruma. Pia alifanya vile ili kuonyesha kama Baba yake, Muumbaji wa uzima, alikuwa amemupatia uwezo juu ya kifo.—Soma Yohana 5:21, 28, 29.

Ufufuo mbalimbali Yesu alifanya unatupatia uhakika juu ya ahadi zake za wakati unaokuja. Yesu atafufua watu wengi sana, kutia ndani watu wasio haki wenye hawakujua kitu chochote juu ya Mungu wa kweli. Watapewa nafasi ya kumujua na kumupenda Yehova Mungu.—Soma Matendo 24:15.