Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 Kichwa| MUNGU ANAKUONA

Mungu Anakuhangaikia?

Mungu Anakuhangaikia?

“Mimi ninateseka nami ni maskini. Yehova mwenyewe ananijali [ao ananihangaikia].” *DAUDI MUFALME WA ISRAELI, ALIYEISHI KATI YA MWAKA WA 1001 NA 1100 MBELE YA KUZALIWA KWA YESU

“Mataifa ni kamatone kutoka katika ndoo [ao mbeketi].”—ISAYA 40:15

Lilikuwa jambo lenye kufaa Daudi afikiri kwamba Mungu anamuhangaikia? Mungu anakuhangaikia wewe? Kwa watu wengi ni vigumu kuamini kwamba Mungu mweza-yote anawahangaikia. Sababu gani?

Sababu moja ni kwamba Mungu ana uzima wa hali ya juu sana tofauti na wanadamu. Anapoonekana kutoka kwenye cheo chake cha juu sana, mataifa mazima “ni kama tone kutoka katika ndoo [ao mbeketi]; nayo yamehesabiwa kuwa kama mavumbi membamba juu ya mizani.” (Isaya 40:15) Mwandishi mumoja wa siku zetu mwenye mashaka juu ya dini alifikia hata kusema kama ni “wazo la hali ya juu sana kuamini kwamba kuna Mungu anayekuhangaikia wewe na kupendezwa mara moja na mambo unayofanya.”

Kwa upande mwengine, watu fulani wanafikiri kwamba Mungu hawezi kuwahangaikia kwa sababu ya mwenendo wao. Kwa mufano, mwanaume mumoja anayeitwa Jim anasema hivi: “Siku zote nilisali ili niwe na amani na sifa ya kujizuia, lakini wakati kwa wakati, hasira yangu ilirudia. Mwishowe, niliamua kwamba nilikuwa mutu mubaya sana na kwamba Mungu hangeweza kunisaidia.”

Je, Mungu iko mbali sana na sisi wanadamu na kwa hiyo anashindwa kutuona? Kwa kweli, anaona namna gani viumbe wake wasiokamilika? Bila Mungu mwenyewe kutupatia ujuzi juu yake, hakuna mwanadamu anayeweza kusema habari juu ya Mungu na kujibu maulizo hayo. Lakini, Biblia, ujumbe wa Mungu ulioongozwa na roho yake kwa ajili ya wanadamu, inatuhakikishia kwamba Mungu haiko mbali sana hivi kwamba asiwahangaikie watu. Biblia inasema hivi: ‘Kweli, haiko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Katika habari ine zinazofuata, tutazungumuzia mambo Mungu anatuambia juu ya namna anahangaikia watu na namna alihangaikia watu kama wewe walioishi kwelikweli.

^ fu. 3 Zaburi 40:17; Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.