Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | TUNA LAZIMA YA MUNGU?

Sababu Gani Tuna Lazima ya Mungu?

Sababu Gani Tuna Lazima ya Mungu?

Waganga ambao wanatunza magonjwa ya akili wanasema kwamba watu hawana lazima tu ya kutosheleza mahitaji yao ya kimwili ili kuwa na furaha ya kweli. Tunaona jambo hilo kwa sababu watu wanapenda wajulikane kuwa washiriki wa kikundi fulani ao kutumikia kusudi ao mutu fulani ambaye ni mukubwa zaidi kuwapita. Ili kutosheleza uhitaji huo, wengine wanapitisha wakati wao wa kujifurahisha kwa kuangalia ao kushugulikia mazingiza, ufundi, muziki, na mambo mengine. Lakini, watu wengi hawapate furaha ya kweli na yenye kudumu kwa kufuatia mambo hayo.

Mungu anapenda wanadamu wawe na furaha sasa na hata milele

Wasomaji wa Biblia hawashangazwe na jambo la kwamba wanadamu wanazaliwa wakiwa na tamaa ya kumuabudu Mungu. Sura za kwanza​-kwanza za kitabu cha Biblia cha Mwanzo zinaonyesha kwamba kisha Mungu kuumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza, alizungumuza nao mara kwa mara, na hivyo akawaruhusu wafanye uhusiano wa kiroho pamoja naye. (Mwanzo 3:8-10) Mungu hakuumba wanadamu ili waishi bila kumutegemea yeye; wana uhitaji wa kupashana habari na Muumbaji wao. Biblia inazungumuzia mara nyingi uhitaji huo.

Kwa mufano, Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Kwa maneno hayo, tunaweza kusema kwamba jambo la maana zaidi ili kuwa na maisha yenye furaha na yenye kurizisha ni kutosheleza tamaa ambayo tulizaliwa nayo ya kumujua Mungu. Tunaweza kufanya hivyo namna gani? Yesu alionyesha jibu la ulizo hilo wakati alisema hivi: ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mukate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’ (Mathayo 4:4) Ni katika njia gani maneno ya Mungu, ni kusema, mawazo na maagizo ya Mungu yaliyo katika Biblia, yanafanya iwezekane tuwe na maisha yenye furaha na yenye kusudi? Acheni tuzungumuzie njia tatu za maana.

Tuna Lazima ya Muongozo Muzuri

Leo, kuna watu wengi wenye elimu na wenye ujuzi wanaotoa mashauri juu ya uhusiano, upendo, maisha ya familia, namna ya kutatua ugomvi, furaha, na hata juu ya kusudi la maisha. Lakini, ni nani anayestahili kabisa kutoa muongozo muzuri na wenye kutumainika juu ya mambo hayo yote isipokuwa tu Muumbaji wa wanadamu, Yehova Mungu?

Kama vile kitabu cha muongozo kwa ajili ya mutumiaji, Biblia ni kitabu cha muongozo kwa ajili ya maisha

Tuchukue mufano: Unaponunua chombo kipya, kama vile kamera ao kompyuta (ordinatere), unakitazamia kikuje na kitabu cha muongozo kutoka kwa mutengenezaji, ambacho kinafasiria namna ya kutumia chombo hicho kwa njia nzuri na ambayo itakuletea furaha. Biblia inaweza kufananishwa na kitabu hicho cha muongozo. Ni kitabu cha muongozo kwa ajili ya maisha ya wanadamu, ambacho Mungu, aliyeanzisha maisha ya wanadamu, ametupatia, sisi watumiaji wa chombo hicho, ni kusema, maisha. “Kitabu hicho cha muongozo kwa ajili ya mutumiaji” kinaeleza ikiwa chombo hicho kimekusudiwa kufanya nini na namna ya kukitumia kwa matokeo mazuri.

Kama vile tu kitabu cha muongozo ambacho kiliandikwa vizuri, Biblia inawaonya watu wanaoisoma juu ya matendo ambayo yanaweza kuharibu maisha. Wengine wanaweza kutupatia mashauri ambayo yanaonekana kuwa mepesi kufuata, lakini ni jambo lenye kupatana na akili kufikiri kwamba tutapata matokeo mazuri na kuepuka matatizo ikiwa tunafuata maagizo ya Muumbaji wetu, sivyo?

‘Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama muto, na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.’​—Isaya 48:17, 18

Katika Biblia, tunaweza kupata muongozo na musaada ambao tunahitaji

Ijapokuwa Yehova Mungu anatupatia maagizo na miongozo, hatulazimishe tuifuate. Lakini, kwa sababu anatupenda na anataka kutusaidia, anatusihi hivi: ‘Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama muto, na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.’ (Isaya 48:17, 18) Kwa kifupi, ikiwa tunafuata muongozo wa Mungu, tutaishi vizuri. Katika maneno mengine, tuna lazima ya Mungu ili kuishi vizuri na kuwa wenye furaha.

Tuna Lazima ya Majibu ya Maulizo Ambayo Tunajiuliza Katika Maisha

Watu fulani wanaona kwamba hawana lazima ya Mungu kwa sababu wana maulizo mengi ambayo yanawasumbua katika maisha, maulizo hayo yanawafanya wasiamini kwamba kuna Mungu mwenye upendo. Kwa mufano, wanaweza kuuliza hivi: ‘Sababu gani watu wazuri wanateseka?’ ‘Sababu gani watoto fulani wasio na kosa wanazaliwa wakiwa na ulemavu?’ ‘Sababu gani maisha yanajaa ukosefu wa haki?’ Hayo ni maulizo mazito, na kupata majibu ya maulizo hayo kunaweza kuwa na matokeo katika maisha yetu. Lakini, kuliko kumulaumu Mungu haraka​-haraka kwa sababu ya matatizo hayo, acheni tuone namna Neno la Mungu, Biblia, linaweza kutusaidia kuelewa jambo hilo.

Sura ya tatu ya kitabu cha Mwanzo inazungumuzia habari ya Shetani, ambaye, katika umbo la nyoka, alijaribu kuwafanya wanadamu wa kwanza wavunje amri ambayo Yehova Mungu aliwapatia kwamba wasikule matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya. Shetani alimuambia Eva hivi: ‘Hakika hamutakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mutakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mutakuwa kama Mungu, mukijua mema na mabaya.’​—Mwanzo 2:16, 17; 3:4, 5.

Kwa maneno hayo, Shetani hakuhakikisha tu kwamba Mungu ni muongo lakini alionyesha pia kwamba namna ya Mungu ya kutawala si ya haki. Ibilisi alipinga kwamba ikiwa wanadamu wanamusikiliza yeye, mambo yatawaendea vizuri. Maulizo hayo hayangejibiwa namna gani? Yehova aliamua kuacha wakati upite ili kuwawezesha wote waone ikiwa mashitaka yaliyotokezwa juu yake yalikuwa ya kweli ao ya uongo. Kwa kufanya hivyo, alikuwa anamupatia Shetani na wale ambao wamemuunga mukono nafasi ya kuonyesha ikiwa wanadamu wanaweza kuishi vizuri bila kumutegemea Mungu.

Unawaza jibu ni gani kwa maulizo ya Shetani? Je, wanadamu wanaweza kuishi vizuri na kujitawala wenyewe kwa matokeo mazuri bila kumutegemea Mungu? Mateso, ukosefu wa haki, magonjwa, kifo, uvunjaji wa sheria, mwenendo mubaya, vita, mauaji makubwa, na mateso mengine ambayo yamewasumbua wanadamu kwa miaka mingi yanaonyesha kabisa kwamba wanadamu wameshindwa kujitawala wenyewe bila kumutegemea Mungu. Biblia haionyeshe kwamba ni Mungu ndiye anawaletea wanadamu matatizo lakini inaonyesha sababu kubwa inayofanya kuwe matatizo hayo kwa kusema hivi: ‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’​—Mhubiri 8:9.

Maneno hayo yanatusaidia kuelewa kwamba tuna lazima ya Mungu ili kupata majibu ya maulizo yenye kusumbua wanadamu na pia ili kutatua matatizo yetu, sivyo? Mungu atafanya nini?

Tuna Lazima ya Musaada wa Mungu

Watu wametamani kwa muda murefu kuishi bila kugonjwa, kuzeeka, na kufa. Wametumia wakati, nguvu, na mali nyingi sana ili kumaliza matatizo hayo, lakini wamepata mafanikio madogo tu ao hata hawapate mafanikio yoyote. Wengine wametumaini kwamba, kwa kutumia muchanganyiko wa dawa mbalimbali, kwa kunywa maji ya aina fulani, ao kwa kuishi mahali fulani, wanaweza kuishi bila kuzeeka. Mambo hayo yote ni ndoto tu zenye kuvunja moyo.

Mungu anataka wanadamu waishi vizuri na wawe na furaha. Hivyo ndivyo Mungu alikusudia mwanzoni alipoumba wanadamu, na hajasahau kusudi hilo. (Mwanzo 1:27, 28; Isaya 45:18) Yehova Mungu anatuhakikishia kwamba jambo lolote ambalo anakusudia kufanya litafanyika bila shaka. (Isaya 55:10, 11) Biblia inatuambia juu ya kusudi la Mungu la kurudisha hali za Paradiso ambazo mwanaume na mwanamuke wa kwanza walipoteza. Katika kitabu cha mwisho cha Biblia, tunapata maneno haya: “Naye [Yehova Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” (Ufunuo 21:4) Namna gani Mungu ataleta hali hizo nzuri, na namna gani tunaweza kufaidika na ahadi hiyo?

Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, aliwafundisha wafuasi wake kusali mapenzi ya Mungu yatendeke. Watu wengi wanajua sala hiyo na wanairudilia​-rudilia, wengine wanaiita Sala ya Bwana. Sala hiyo inasema hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Kwa kweli, Ufalme wa Mungu ni njia ambayo Yehova Mungu atatumia ili kuondoa mambo yenye kuhuzunisha ambayo yametokana na utawala wa wanadamu na kuleta dunia mupya ya haki ambayo aliahidi. * (Danieli 2:44; 2 Petro 3:13) Tunaweza kufanya nini ili tufaidike na ahadi ya Mungu?

Yesu Kristo anaonyesha jambo rahisi ambalo tunapaswa kufanya kwa kusema hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Kwa kweli, kwa musaada wa Mungu, inawezekana kuishi milele katika dunia mupya iliyoahidiwa. Tumaini kama hilo linaweza kukuhakikishia sababu nyingine ya kujibia ndiyo kwa ulizo, Tuna lazima ya Mungu?

Tuna Lazima Kabisa ya Kumutafuta Mungu

Miaka elfu mbili iliyopita, kwenye Aeropago, ao Kilima cha Mars, huko Athene, mutume Paulo alisema hivi juu ya watu wa Athene ambao walikuwa na mawazo mengi na ambao walikuwa tayari kukubali mawazo ya wengine: “Yeye mwenyewe huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote. Kwa maana kupitia kwake tuna uhai na tunaenda na kuwako, hata kama vile ambavyo watu fulani ambao ni washairi kati yenu wamesema, ‘Kwa maana sisi pia ni uzao wake.’”​—Matendo 17:25, 28.

Mambo ambayo Paulo alisema juu ya watu wa Athene bado ni ya kweli. Muumbaji wetu anatutolea hewa ambayo tunapumua, chakula ambacho tunakula, na maji ambayo tunakunywa. Haingewezekana tuishi bila mambo hayo mazuri ambayo Yehova ametupatia ili kutegemeza uzima wetu. Lakini, sababu gani Mungu ameendelea kuwapatia watu wote mambo hayo, iwe wanamuamini ao hapana? Paulo alisema kwamba ni ‘ili wao wamutafute Mungu, ikiwa wangeweza kupapasa-papasa wakimutafuta na kwa kweli wamupate, ijapokuwa, kweli, hayuko mbali sana na kila mumoja wetu.’​—Matendo 17:27.

Je, ungependa kumujua Mungu vizuri, ni kusema, kujifunza mengi juu ya makusudi yake na shauri ambalo anatupatia ili kuishi vizuri leo na hata milele? Ikiwa jibu lako ni ndiyo, tunakuomba uzungumuze na mutu ambaye alikuletea gazeti hili ao uandikie wachapishaji wa gazeti hili. Watafurahi kukusaidia.

^ Ili kupata habari zaidi juu ya namna Ufalme huo utakavyofanya mapenzi ya Mungu yatendeke duniani, soma sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza kusoma kitabu hicho ao kukichukua kwenye adresi yetu ya Internete www.isa4310.com.