Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPUNGUZA HATARI YA KUPATA MAGONJWA

Ujilinde ili Usipate Magonjwa

Ujilinde ili Usipate Magonjwa

MAJIJI mengi ya zamani yalikuwa yanalindwa na kuta kubwa-kubwa. Kama adui angetoboa nafasi moja tu katika ukuta na kuingia, usalama wa muji wote ungekuwa katika hatari. Mwili wako uko kama muji wenye kuzungukwa na kuta. Kama unajilinda muzuri utakuwa na afya ya muzuri, lakini kama haujilinde muzuri afya yako itakuwa katika hatari. Ona mambo tano yenye yanaweza kukuweka katika hatari ya kupata magonjwa, na namna unaweza kufanya ili kujilinda muzuri zaidi.

1 MAJI

HATARI: Mikrobe yenye kuwa hatari inaweza kuingia katika mwili wako kupitia maji machafu.

NAMNA YA KUJILINDA: Namna ya muzuri zaidi ya kujilinda ni kuhakikisha kama mahali unashotea maji hapachafuliwe. Ikiwa unajua ao unawazia kama mahali unashotea maji pamechafuliwa, unaweza kufanya maji hayo yakuwe safi wewe mwenyewe nyumbani. * Weka maji safi katika chombo chenye kufunikwa, na ili usichafue maji hayo wakati unapenda kupatia watu wengine, tumia jagi yenye kuwa safi ao robinet. Usiweke hata siku moja mikono yako katika chombo chenye kuwa safi ambamo unawekea maji. Kama inawezekana, ujikaze kuishi katika eneo lenye uchafu wa WC hauchafue maji.

2 CHAKULA

HATARI: Mikrobe yenye kuwa hatari inaweza kuwa katika ao kwenye chakula chako.

NAMNA YA KUJILINDA: Chakula chenye kuwa na mikrobe kinaweza kuonekana kuwa kizuri na chenye kujenga mwili. Kwa hiyo, kila wakati ujikaze kusafisha muzuri sana mboga na matunda yote. Hakikisha kwamba mafiga na vyombo vyenye unatumia wakati unapika vyote viko safi, pia hakikisha kwamba mikono yako iko safi wakati unapika ao wakati unapatia watu wengine chakula. Inaomba kupika vyakula fulani kwa muda murefu ao kwa kutumia moto mingi ili kuua mikrobe hatari. Usikule chakula chenye kimepoteza rangi yake ya kawaida ao chakula chenye kuwa na harufu ya mubaya ao chenye hakifurahishe wakati unakionja; alama hizo zinaonyesha kama chakula hicho kiko na mikrobe. Bila kukawia, tia katika nafasi ya baridi chakula chenye hautumie. Uepuke kupikia wengine chakula wakati uko mugonjwa. *

3 VIDUDU

HATARI: Vidudu fulani vinaweza kukuambukiza mikrobe hatari yenye kuwa katika mwili wao.

NAMNA YA KUJILINDA: Ubakie ndani ya nyumba ili usiambukizwe na vidudu vyenye kuwa na magonjwa wakati vinapita-pita ao uvae nguo zenye zinaweza kukulinda, kama vile nguo za mikono murefu na suruali (pantalons). Lala ndani ya chandarua (moustiquaires) cha kuzuia vidudu, na tumia dawa ya kuua vidudu. Ondoa maji yenye kusimama nafasi moja kwenye imbu wanaweza kuzaana. *

4 WANYAMA

HATARI: Mikrobe fulani yenye kuishi katika mwili wa munyama bila kuwa hatari kwake, inaweza kutia afya yako katika hatari. Ikiwa munyama fulani anakuuma ao kukukwaruza ao ikiwa mwili wako uligusa mavi yake, unaweza kuwa katika hatari.

NAMNA YA KUJILINDA: Watu fulani wanaamua kuweka wanyama wao inje ya nyumba ili waepuke kuwa nao kila wakati. Nawa mikono kisha kugusa munyama fulani wa nyumbani, na uepuke kabisa kukaribia sana wanyama wa pori. Kama munyama fulani anakuuma ao kukukwaruza, safisha muzuri mahali alikuumiza na uonane na munganga. *

5 WATU

HATARI: Mikrobe fulani inaweza kuingia katika mwili wako kupitia matone kidogo ya mate ya mutu mwengine wakati anakohoa ao anapiga chafya. Unaweza pia kuambukizwa wakati ngozi yako inagusa ngozi ya mutu mwengine, kwa mufano kupitia kusalimiana kwa mukono ao kukumbatiana. Mikrobe yenye kutoka kwa watu wengine inaweza kujificha kwenye vitu kama vile mulango, mahali fulani pa kukamatia, telefone, télécommandes, ao kwenye ordinatere na claviers za ordinatere.

NAMNA YA KUJILINDA: Usichangie na mutu mwengine vitu kama vile wembe, brosse ya meno, ao nguo ya kujipanguza nayo maji kwenye mwili. Epuka kabisa umaji-maji fulani wenye kutoka katika mwili wa wanyama ao wa watu wengine, kutia ndani damu na vitu vingine vyenye kuwa na damu. Usizarau faida yenye unaweza kupata ikiwa unanawa mikono yako muzuri sana na kila wakati. Pengine hiyo ndiyo njia ya muzuri zaidi ya kuzuia maambukizo yasienee.

Kama inawezekana, bakia nyumbani wakati uko mugonjwa. Shirika moja la Amerika linapendekeza kwamba ni muzuri kutumia mouchoir wakati unakohoa ao kupiga chafya, lakini usifanye hivyo katika mikono yako. (Centers for Disease Control and Prevention)

Mezali moja ya zamani inasema hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha.’ (Methali 22:3) Maneno hayo ni ya kweli kabisa leo katika dunia hii yenye kujaa magonjwa yenye yanaweza kuwa hatari! Kwa hiyo, zungumuza na munganga fulani wa eneo lenu ili kupata mashauri, na wewe mwenyewe ujilinde na hatari ya kupata magonjwa kwa kujikaza kuwa musafi. Ujilinde zaidi, na upunguze hatari ya kupata magonjwa!

^ fu. 6 Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linapendekeza mambo mbalimbali yenye mutu anaweza kufanya nyumbani ili maji yakuwe safi. Kwa mufano, kutia klorini katika maji, kutia maji kwenye jua, kuyachuya, ao kuyatokotesha.

^ fu. 9 Ili kupata habari zingine juu ya namna ya kulinda chakula, soma Amuka! ya Mwezi wa 6, 2012 ukurasa wa 3-9.

^ fu. 12 Ili kujua namna mbalimbali ya kujilinda ili usipate malaria, soma Amuka! ya Mwezi wa 7, 2015 ukurasa wa 14-15.

^ fu. 15 Mara nyingi kama mutu anaumizwa na kiumbe fulani mwenye sumu anapaswa kutafuta matunzo bila kukawia.