Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuzungumuzia Matatizo

Namna ya Kuzungumuzia Matatizo

MAGUMU

Wakati munazungumuzia tatizo fulani katika ndoa yenu, munajisikia mubaya zaidi kisha tu kuzungumuzia tatizo hilo? Kama jibu ni ndiyo, munaweza kufanya hali ikuwe muzuri. Kwanza, munapaswa kujua kwamba bibi na bwana wanazungumuzia matatizo kwa njia tofauti. *

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Kuliko kusikiliza namna ya kumaliza tatizo fulani, wanawake wanazoea kuzungumuzia tatizo hilo. Kwa kweli, wakati fulani kuzungumuza ni jambo lenye linasaidia.

“Ninajisikia muzuri zaidi wakati ninaeleza namna ninajisikia na kuona kwamba bwana yangu ananielewa. Kisha tu kufanya hivyo, ninajisikia muzuri sana.”—Sirppa. *

“Ni vigumu kusahau matatizo yangu kama sijamuelezea bwana yangu namna ninajisikia kabisa. Wakati ninasema mambo yangu yote, yanaacha kunisumbua.”—Ae-Jin.

“Kuzungumuzia tatizo, ni kama kazi ya kuvumbua. Wakati ninazungumuzia tatizo langu, ninachunguza tatizo hilo kwa uangalifu na kufikia kujua namna lilianza.”—Lurdes.

Mara nyingi wanaume wanawaza namna ya kumaliza matatizo. Hilo linaeleweka kwa sababu wakati mwanaume anamaliza tatizo fulani anajisikia kuwa wa maana. Wakati bwana anaonyesha namna ya kumaliza tatizo fulani ni njia ya kuonyesha kwamba bibi yake anaweza kumutumainia ili kupata musaada. Kwa hiyo, wanaume wanajisikia mubaya wakati bibi zao hawako tayari kukubali mawazo yao kuhusu namna ya kumaliza tatizo fulani. Bwana mumoja mwenye kuitwa Kirk anasema hivi: “Siwezi kuelewa sababu gani mutu anaweza kuzungumuzia tatizo fulani bila kuwa na lazima ya kujua namna ya kumaliza tatizo hilo!”

Kitabu kimoja kinasema hivi: “Mbele ya kutoa shauri, unapaswa kwanza kuelewa tatizo. Unapaswa kumuonyesha bibi yako kwamba unamuelewa na kwamba unajitia pa nafasi yake mbele ya kumuambia namna ya kumaliza tatizo hilo. Mara nyingi, bibi yako hakuombe umuambie namna ya kumaliza magumu yake, anapenda tu umusikilize muzuri.”—Les couples heureux ont leurs secrets. Les sept lois de la réussite.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Kwa bwana: Ukuwe na tabia ya kusikiliza kwa uangalifu. Mwanaume mumoja mwenye kuitwa Tomás anasema hivi: “Wakati fulani kisha kusikiliza ninajiambia, ‘Hilo halikutimiza kitu.’ Lakini hilo ndilo jambo lenye bibi yangu anapenda; anapenda nimusikilize.” Mwanaume mwenye kuitwa Stephen, anaunga mukono mawazo ya Tomás. Anasema hivi: “Ninaona kwamba ni muzuri zaidi kumuacha bibi yangu aseme bila kumukatiza. Mara nyingi, wakati anamaliza kusema, ananiambia kwamba anajisikia muzuri zaidi.”

Jaribu kufanya hivi: Wakati utakuwa tena na nafasi ya kuzungumuzia tatizo fulani pamoja na bibi yako, uepuke kutoa shauri lenye hakukuomba. Umuangalie wakati anazungumuza, na ukaze akili juu ya mambo yenye anasema. Utikise kichwa ili kuonyesha kwamba unakubali. Rudilia kwa kifupi mambo yote yenye amesema ili kuonyesha kwamba umeelewa. Mwanaume mumoja mwenye kuitwa Charles anasema hivi: “Wakati fulani bibi yangu anapenda tu kujua kwamba ninamuelewa na kwamba ninamuunga mukono.”—Kanuni ya Biblia: Yakobo 1:19.

Kwa bibi: Useme mambo yenye unapenda bwana yako akufanyie. Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Eleni anasema hivi: “Tunapenda bwana zetu wajue mambo yenye tuko nayo lazima, lakini wakati fulani tunapaswa kusema mambo waziwazi.” Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Ynez anasema hivi: “Ninaweza kusema, ‘Jambo fulani linanisumbua, na ninapenda unisikilize. Sipendi unionyeshe namna ya kumaliza jambo hilo, lakini ninapenda ujue namna ninajisikia.’”

Jaribu kufanya hivi: Kama bwana yako anakuonyesha namna ya kumaliza tatizo fulani bila kukusikiliza kwanza, usiseme mara moja kwamba hakuhangaikie. Pengine anajaribu kukupunguzia muzigo. Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Ester anasema hivi: “Kuliko kukasirika, ninajikaza kutambua kwamba bwana yangu ananihangaikia na kwamba ananisikiliza, lakini pia anapenda tu kunisaidia.”—Kanuni ya Biblia: Waroma 12:10.

Kwa bibi na bwana: Mara nyingi tunatendea wengine namna tunapenda watutendee. Lakini, ili kuzungumuzia muzuri matatizo, unapaswa kufikiria namna bibi ao bwana yako angependa umutendee. (1 Wakorintho 10:24) Bwana mumoja mwenye kuitwa Miguel anasema hivi: “Kama uko bwana, ukuwe tayari kusikiliza. Kama uko bibi, wakati fulani ni muzuri ukuwe tayari kusikiliza wakati bwana yako anakuonyesha namna ya kumaliza tatizo. Wakati munaelewana, munapata faida.”—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 3:8.

^ fu. 4 Pengine mambo yenye tutazungumuzia katika habari hii hayatatumika kwa kila bwana ao bibi. Lakini, kanuni zenye tutazungumuzia zinaweza kusaidia kila mutu ajue namna ya kuzungumuza muzuri zaidi pamoja na bibi ao bwana yake.

^ fu. 7 Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.